Friday, July 8, 2011

Haye atakiwa marekani

Haye atakiwa Marekani
Friday, 08 July 2011 06:41
LOS ANGELES, Marekani

DAVID Haye, ameambiwa aende kupigana Marekani ili apate mafanikio kama bondia mwingine wa Uingereza, Amir Khan.Khan alikwenda kufanya mazoezi Marekani na akaja kuwa bingwa wa dunia baada ya kwenda Hollywood na kufanyishwa mazoezi na kocha mahiri wa Kimarekani, Freddie Roach.

Mtu maarufu katika ngumi, Richard Schaefer, anaamini kuwa kipaji cha Haye kinaweza kuzaliwa upya baada ya kupoteza pambano lake la uzito wa juu duniani kwa kupigwa kwa pointi dhidi ya Wladimir Klitschko, mjini Hamburg, Jumamosi usiku.

Haye sasa anataka kurudiana na Klitschko au kutwangana na kaka yake Vitali, ambaye ni bingwa wa mkanda wa WBC .

Lakini Schaeffer, ambaye ni Mtendaji Mkuu wa kampuni ya promosheni ya Oscar De La Hoya, Golden Boy, ambaye ni promota wa Khan na Haye alisema, "anatakiwa kuja na kupigana mapambano Marekani kwa mara ya kwanza.

"David hakuweza kucheza vizuri Jumamosi na sikufurahishwa na uchezaji wake.

"Lakini si sahihi kumjaji David kwa uchezaji wa mechi moja. Ana umri wa miaka 30 na bado ni mzuri, ni mpiganaji anayefurahisha katika uzito.

"Hakuna anayejali kuhusu akina Klitschkos."

Wakati huohuo, Schaefer, amesema Khan anaweza kujiandaa kupigana kwa ajili ya kutwangana na Floyd  Mayweather mwakani.

Bingwa wa mkanda wa WBA, Khan, ameanza maandalizi ya kucheza pambano la kuunganisha mataji dhidi ya Zab Judah mjini Las Vegas, Julai 23.

Pambano lake linalofuatia linaweza kuwa dhidi ya Erik Morales, Desemba na kisha kurejea Uingereza ambapo bondia huyo mwenye miaka 24, atahamia katika uzani wa welter na anaweza kutwangana na Kell Brook.

Huenda akatwanga na  Mayweather Novemba 2012.

Schaefer alisema: "Hii ni mipango mikubwa kwa Khan.

"Nimekuwa na mazungumzo na Mayweather na yuko tayari kutwangana na Amir."
 
Haye atakiwa Marekani
Friday, 08 July 2011 06:41
LOS ANGELES, Marekani

DAVID Haye, ameambiwa aende kupigana Marekani ili apate mafanikio kama bondia mwingine wa Uingereza, Amir Khan.Khan alikwenda kufanya mazoezi Marekani na akaja kuwa bingwa wa dunia baada ya kwenda Hollywood na kufanyishwa mazoezi na kocha mahiri wa Kimarekani, Freddie Roach.

Mtu maarufu katika ngumi, Richard Schaefer, anaamini kuwa kipaji cha Haye kinaweza kuzaliwa upya baada ya kupoteza pambano lake la uzito wa juu duniani kwa kupigwa kwa pointi dhidi ya Wladimir Klitschko, mjini Hamburg, Jumamosi usiku.

Haye sasa anataka kurudiana na Klitschko au kutwangana na kaka yake Vitali, ambaye ni bingwa wa mkanda wa WBC .

Lakini Schaeffer, ambaye ni Mtendaji Mkuu wa kampuni ya promosheni ya Oscar De La Hoya, Golden Boy, ambaye ni promota wa Khan na Haye alisema, "anatakiwa kuja na kupigana mapambano Marekani kwa mara ya kwanza.

"David hakuweza kucheza vizuri Jumamosi na sikufurahishwa na uchezaji wake.

"Lakini si sahihi kumjaji David kwa uchezaji wa mechi moja. Ana umri wa miaka 30 na bado ni mzuri, ni mpiganaji anayefurahisha katika uzito.

"Hakuna anayejali kuhusu akina Klitschkos."

Wakati huohuo, Schaefer, amesema Khan anaweza kujiandaa kupigana kwa ajili ya kutwangana na Floyd  Mayweather mwakani.

Bingwa wa mkanda wa WBA, Khan, ameanza maandalizi ya kucheza pambano la kuunganisha mataji dhidi ya Zab Judah mjini Las Vegas, Julai 23.

Pambano lake linalofuatia linaweza kuwa dhidi ya Erik Morales, Desemba na kisha kurejea Uingereza ambapo bondia huyo mwenye miaka 24, atahamia katika uzani wa welter na anaweza kutwangana na Kell Brook.

Huenda akatwanga na  Mayweather Novemba 2012.

Schaefer alisema: "Hii ni mipango mikubwa kwa Khan.

"Nimekuwa na mazungumzo na Mayweather na yuko tayari kutwangana na Amir."
 
DAVID Haye, ameambiwa aende kupigana Marekani ili apate mafanikio kama bondia mwingine wa Uingereza, Amir Khan.Khan alikwenda kufanya mazoezi Marekani na akaja kuwa bingwa wa dunia baada ya kwenda Hollywood na kufanyishwa mazoezi na kocha mahiri wa Kimarekani, Freddie Roach.

Mtu maarufu katika ngumi, Richard Schaefer, anaamini kuwa kipaji cha Haye kinaweza kuzaliwa upya baada ya kupoteza pambano lake la uzito wa juu duniani kwa kupigwa kwa pointi dhidi ya Wladimir Klitschko, mjini Hamburg, Jumamosi usiku.

Haye sasa anataka kurudiana na Klitschko au kutwangana na kaka yake Vitali, ambaye ni bingwa wa mkanda wa WBC .

Lakini Schaeffer, ambaye ni Mtendaji Mkuu wa kampuni ya promosheni ya Oscar De La Hoya, Golden Boy, ambaye ni promota wa Khan na Haye alisema, "anatakiwa kuja na kupigana mapambano Marekani kwa mara ya kwanza.

"David hakuweza kucheza vizuri Jumamosi na sikufurahishwa na uchezaji wake.

"Lakini si sahihi kumjaji David kwa uchezaji wa mechi moja. Ana umri wa miaka 30 na bado ni mzuri, ni mpiganaji anayefurahisha katika uzito.

"Hakuna anayejali kuhusu akina Klitschkos."

Wakati huohuo, Schaefer, amesema Khan anaweza kujiandaa kupigana kwa ajili ya kutwangana na Floyd  Mayweather mwakani.

Bingwa wa mkanda wa WBA, Khan, ameanza maandalizi ya kucheza pambano la kuunganisha mataji dhidi ya Zab Judah mjini Las Vegas, Julai 23.

Pambano lake linalofuatia linaweza kuwa dhidi ya Erik Morales, Desemba na kisha kurejea Uingereza ambapo bondia huyo mwenye miaka 24, atahamia katika uzani wa welter na anaweza kutwangana na Kell Brook.

Huenda akatwanga na  Mayweather Novemba 2012.

Schaefer alisema: "Hii ni mipango mikubwa kwa Khan.

"Nimekuwa nazungumza na myweather na yuko tayari kutwangana na Amir

No comments:

Post a Comment