Monday, June 27, 2011

Bob Junior Ndani ya Bifu na Wema Sepetu

Bob Junior Ndani ya Bifu na Wema Sepetu Ni kama vile Bob 'Rais wa Masharubaro' Junior ameamua kuingia kwenye 'mapambano' na kila anayekutana naye. Kutoka kwenye blogu ya Bongo Star Link, Dj Choka anatufahamisha ifuatavyo;
Habari nilizozipata mida hii kutoka kwa Rais wa Masharobaro Bob Junior ni kwamba kesho asubuhi ameitwa kituo cha Police pale Ostabey yeye na Wema Sepetu. Kisa hicho ni kwamba leo mchana Wema alienda kituoni pale kwenda kumchukulia Bob Junior RB yake hatimaye Wema akaingizwa yeye ndani kituoni hapo na kuambiwa kuwa alikuwa anatafutwa na Police.

Kisa cha Bob Junior kumpeleka Wema police ni matusi ambayo ametukanwa na Wema na yeye akawa na ushahidi wa kumrekodi na kuipeleka sauti hiyo ya matusi police na kumchukulia RB.

No comments:

Post a Comment