Friday, September 16, 2011

Kutumia kondom ya wanaume


kondom
Kondom ya wanaume
Mimi mvulana, mimi ni mwanamme nieleze jinsi ya kutumia kondom ya wanaume?
  • Hakikisha umeangalia mda wa matumizi wa kondom uliyonayo. Kama mda wake (expiry date) wa matumizi umekwisha basi haikufai. Fungua kipakiti chenye kondomu wakati tu ukiwa tayari kuitumia. Bila hivyo yale mafuta mafuta maalum kwenye kondomu yatakauka.
  • Unapofungua pakiti kuwa mwangalifu usiipasue, au kuitoboa wala kuiharibu kondom yenyewe. Ikipasuka itupilie mbali na uchukue nyingine.
  • Kondomu huwa zimesokotwa na kuwa kama duara. Kuivaa, ile sehemu ya mafuta mafuta inapaswa kuwa nje.
  • Hivyo basi ivae kwa kuikunjua kuanzia kwenye ncha (kichwa)cha uume.
  • Ishike sehemu ya chuchu ya kondomu kwa kutumia dole gumba na kidole chako cha kwanza ili kutoa hewa kutoka sehemu hiyo, ili manii yahifadhiwe mahali hapo pale yatakapotoka.
  • Sasa Endelea kuishikilia kondom kwa mkono mmoja. Kwa kutumia mkono wa pili ikunjue hadi kufikia kwenye mavuzi yaani kwenye shina la uume. Kama mtumiaji hajatahiriwa anapaswa kuvuta lile govi la uume wake kabla ya kuvaa kondomu. Kama kondomu haina kilainishi cha kutosha, vilainishi au majimaji (kama vile silicone, glycerine, au K-Y jelly) vyaweza kuongezwa kwa nje. Tahadhari mafuta kama yale ya kupikia, ya kujipaka mwilini kama kama vile Vaseline hayafai kutumiwa kama kilainishi.
  • Baada ya kufanya mapenzi kondomu inapaswa kuvuliwa kwa njia sahihi pia. Baada tu ya kufika kilele na kutoa manii, mwanaume anapaswa kuutoa uume wake kutoka ukeni, kabla haujalegea kabisa, kwani akichelewa huenda kondom ikatumbukia ukeni mwa mwanamke. Kisha ashikilie kondomu kutoka shinani mwa uume na kuivua taratibu pasi na manii kumwagika.
  • Unaweza kuifunga kondom kwenye karatasi na kuitupa kwenye choo cha shimo
  • Usitupe kondom kwenye hooni cha kupiga maji kwani huenda ikatatiza utendaji kazi wa choo hicho.
  • Tumia kondom nyengine kwa kila tendo jengine la kujamiana. Tumia kondom kila wakati unapofanya mapenzi.

Wednesday, August 24, 2011

Nasri aenda Man City

 Nasri
Manchester City wamekubaliana na Arsenal kumsajili kiungo Samir Nasri. Nasri sasa anaelekea mjini Manchester kwa ajili ya vipimo vya afya.
 
Nasri

Nasri alifanya mazoezi na Arsenal siku ya Jumanne asubuhi kujiandaa na mchezo wa Klabu Bingwa Ulaya dhidi ya Udinese, utakaochezwa Jumatano. Hata hivyo jina lake liliondolewa kwenye orodha ya wachezaji.
Kiungo huyo kutoka Ufaransa anakwenda Manchester pia kukamilisha mkataba wake ambao unadhaniwa kuwa na thamani ya pauni milioni 25.
Meneja wa City, Roberto Mancini alisema siku ya Jumapili kuwa anataka kumsajili Nasri ndani ya kipindi cha saa 48.
Nasri aenda Man City
Manchester City wamekubaliana na Arsenal kumsajili kiungo Samir Nasri. Nasri sasa anaelekea mjini Manchester kwa ajili ya vipimo vya afya
Nasri alifanya mazoezi na Arsenal siku ya Jumanne asubuhi kujiandaa na mchezo wa Klabu Bingwa Ulaya dhidi ya Udinese, utakaochezwa Jumatano. Hata hivyo jina lake liliondolewa kwenye orodha ya wachezaji.

Kiungo huyo kutoka Ufaransa anakwenda Manchester pia kukamilisha mkataba wake ambao unadhaniwa kuwa na thamani ya pauni milioni 25.

Meneja wa City, Roberto Mancini alisema siku ya Jumapili kuwa anataka kumsajili Nasri ndani ya kipindi cha saa 48.

Uholanzi yaipiku Hispania ubora wa soka

Uholanzi imeipiku Hispania katika nafasi ya kwanza ya ubora Fifa wa kusakata soka duniani, huku Englan ikipanda nafasi mbili juu hadi ya nne.
Wachezaji wa Uholanzi
Wachezaji wa Uholanzi

Hispania mabingwa wa soka duniani na Ulaya, wameporomoka hadi nafasi ya pili baada ya kupoteza pointi katika mchezo wa kirafiki dhidi ya Italia.
England, licha ya mchezo wake wa kirafiki dhidi ya Uholanzi kuahirishwa, imepanda kwa sababu Brazil ilifungwa na Ujerumani.
Jamhuri ya Ireland imepaa nafasi mbili hadi ya 31, Scotland imeruka nafasi sita na sasa inashikilia nafasi ya 55, Ireland Kaskazini nayo imefanikiwa kwenda nafasi tatu zaidi hadi ya 59, lakini Wales imeporomoka hadi nafasi ya 117.
Kwa kushika nafasi hiyo ya kwanza kwa mara ya kwanza, Uholanzi inakuwa ni taifa la saba kushikilia nafasi hiyo ya juu kisoka duniani zikiwemo - Argentina, Brazil, Ufaransa, Ujerumani na Italia ambazo ziliwahi kukalia kiti hicho.
Hispania ilikuwa inashikilia nafasi ya juu tangu mwezi wa Julai mwaka 2010 kufuatia ushindi walioupata wa Kombe la Dunia dhidi ya Uholanzi nchini Afrika Kusini.
Ujerumani inashikilia nafasi ya tatu, wakati Uruguay ndiyo nchi ya Amerika Kusini iliyo nafasi ya juu kwa dunia ikishika nafasi ya tano kutokana na kushinda Kombe la Copa America hivi karibuni nchini Argentina, wakati Brazil ipo nafasi ya sita.
Italia, Ureno, Argentina na Croatia wamefanikiwa kushikilia nafasi 10 za juu.
Viwango vya ubora wa soka vya Fifa vinatokana na kukusanya matokeo, umuhimu wa mechi zilizochezwa na ubora wa timu pinzani.

Thursday, July 14, 2011

Eritrean Red Sea FC footballers 'disappear' in Tanzania


Thirteen members of an Eritrean football team have failed to return home after a regional tournament in Tanzania, officials say.
After Red Sea FC lost the Cecafa championship semi-final on Saturday, only half of the team turned up for the return flight to Eritrea.
This is said to be the fourth time Eritrean footballers have disappeared.
Young Eritreans often try to escape poverty, a repressive government and national military service.
Tanzania Football Federation (TFF) Angetile Osiah told Reuters news agency that the matter had been reported to the law enforcement authorities to investigate.
"Some team members colluded in the incident by trying to stamp the passports of the missing players at airport immigration checkpoints but when a physical head count was conducted, it was discovered that 13 players were missing," he said.
Tanzania's Young Africans beat their rivals Simba 1-0 in Sunday's Cecafa final.

ROSTAM AZIZ Ajivua Ubunge Na Ujumbe wa NEC ya CCM.

 


ROSTAM ametangaza uamuzi huo katika mkutano uliofanyika IGUNGA  Jumatano wiki hii  ambapo amesema hatua hiyo haitokani na kile alichokiita kuwa ni shinikizo ndani ya chama, bali ni dhamira yake binafsi ikiwa na lengo la kutoa fursa kwa watu wengine kushika nyadhifa hizo alizoziacha.
Alitangaza uamuzi huo katika mkutano  uliofanyika huko IGUNGA TABORA ambapo pamoja na mambo mengine alieleza historia yake katika uongozi ndani ya CCM ukiwemo ubunge wa jimbo la IGUNGA alioushika tangu mwaka 1995 huku akitaja mafanikio na changamoto alizokumbana nazo.
Baadhi ya watu waliokuwa wamehudhuria mkutano huo  walijaribu kumsihi  AZIZ abadili uamuzi wake, suala ambalo alilipinga na kuendelea kushikiria msimamo wake.
Hata hivyo ofisi za Bunge kupitia kwa Kaimu Katibu wake JOHN JOEL zimesema hazina taarifa.
Safari ya siasa ya ROSTAM AZIZ ndani ya bunge ilianzia mwaka 1995 katika uchaguzi mkuu wa kwanza chini ya mfumo wa vyama vingi vya siasa ambapo aliibuka mshindi katika jimbo la IGUNGA.
Mwaka 2000 vile vile alitetea kiti chake cha ubunge na mwaka jana alishiriki katika kinyang’anyiro na katika mkutano wa kampeni wa mgombea wa kiti cha Urais kupitia CCM, Dkt. JAKAYA KIKWETE, aliweza kunadiwa.
Ndani ya Chama Cha Mapinduzi, ROSTAM aliwahi kuwa mjumbe wa Kamati Kuu ya halmashauri kuu ya taifa ya chama hicho, mjumbe wa NEC na mweka hazina.
Mwishoni mwa kikao cha halmashauri kuu ya taifa ya CCM kilichofanyika mjini DODOMA mwezi Aprili mwaka huu, Kamati Kuu ilijiuzulu na hivyo kutoa nafasi ya kuundwa kwa Kamati Kuu nyingine ambamo ROSTAM na wajumbe wengine kadhaa waliachwa
Mwanasiasa huyu pia ni mfanyabiashara ambapo kwa mujibu wa taarifa zilizochapishwa katika tovuti ya Bunge, Rostam ni Mkurugenzi katika kampuni za African Tanneries, Caspian construction, African Trade Development na katika kampuni ya Research on Business yeye ni Mkurugenzi Mtendaji.
Halikadhalika tovuti hiyo inaonyesha kuwa kielimu, ROSTAM ana shahada ya kwanza ya Uchumi
Mbunge wa IGUNGA kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi ROSTAM AZIZ
Mbunge wa IGUNGA kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi ROSTAM  AZIZ ametangaza kuachia nafasi za uongozi wa kisiasa alizokuwa akishikilia ukiwemo ubunge wa jimbo la IGUNGA mkoani TABORA ambao ameushikilia kwa takribani miaka 15  pamoja na ujumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho.

Wednesday, July 13, 2011

EPIQ NATION YAFANA COCOBEACH


Jumapili, iliyopita kampuni ya Simu za Mkononi ya Zantel kupitia Bidhaa yake mpya ya EPIQ NATION iliandaa tamasha kabambe la muziki pale Coco beach kwa ajili ya vijana. 
Wasanii mbalimbali walikuwepo kutoa burudani ikiwemo Mwasiti, Diamond, Chidi Benz na Nameless Kutoka Kenya. Pia kulikuwa na ma underground kibao waliopewa fursa ya kuonyesha vipaji vyao vya kuimba, kuchana pamoja na kudansi Diamond akiwa jukwaani

Saturday, July 9, 2011

Afrika yapata taifa jipya la Sudan Kusini

sherehe Sudan Kusini
Jumamosi hii Julai 9 mwaka 2011 ni siku itakayoingia katika vitabu vya historia kote duniani baada ya machafuko ya takriban miongo miwili hatimaye moja ya nchi kubwa kabisa barani Afrika Sudan inagawanywa rasmi mapande mawili Kaskazini inayosalia kuwa Sudan na taifa jipya linalozaliwa Sudan Kusini. Umoja wa Mataifa , Jumuiya ya kimataifa , Wahisani, Mashirika ya Umoja wa Mataifa na dunia nzima imeelekeza macho na masikio Juba mji mkuu wa taifa la 54 barani Afrika na Sudan yote kwa jumla , kuona historia ikiandikwa lakini kubwa zaidi nini kitakachofuata baada ya kujitawala.
Umoja wa Mataifa umejiandaa vilivyo kuhakikisha usalama umedumishwa ukizingatiwa kuna changamoto nyingi katika taifa hilo lililosambaratika na machafuko ambapo hadi sasa suala la Kordofan Kusini na Abyei yaliyoko mpakani yanatia mashaka. Kuchambua kwa kina histotia hii, matarajio na changamoto , mkuu wa idhaa hii Flora Nducha amezungumza na Dr Salim Ahmed Salim anayeifahamu vilivyo historia ya Sudan, aliyewai kuwa Katibu mkuu wa Umoja wa Afrika na mpatanishi maalum wa Umoja wa Afrika katika mzozo wa Darfur.

Friday, July 8, 2011

Haye atakiwa marekani

Haye atakiwa Marekani
Friday, 08 July 2011 06:41
LOS ANGELES, Marekani

DAVID Haye, ameambiwa aende kupigana Marekani ili apate mafanikio kama bondia mwingine wa Uingereza, Amir Khan.Khan alikwenda kufanya mazoezi Marekani na akaja kuwa bingwa wa dunia baada ya kwenda Hollywood na kufanyishwa mazoezi na kocha mahiri wa Kimarekani, Freddie Roach.

Mtu maarufu katika ngumi, Richard Schaefer, anaamini kuwa kipaji cha Haye kinaweza kuzaliwa upya baada ya kupoteza pambano lake la uzito wa juu duniani kwa kupigwa kwa pointi dhidi ya Wladimir Klitschko, mjini Hamburg, Jumamosi usiku.

Haye sasa anataka kurudiana na Klitschko au kutwangana na kaka yake Vitali, ambaye ni bingwa wa mkanda wa WBC .

Lakini Schaeffer, ambaye ni Mtendaji Mkuu wa kampuni ya promosheni ya Oscar De La Hoya, Golden Boy, ambaye ni promota wa Khan na Haye alisema, "anatakiwa kuja na kupigana mapambano Marekani kwa mara ya kwanza.

"David hakuweza kucheza vizuri Jumamosi na sikufurahishwa na uchezaji wake.

"Lakini si sahihi kumjaji David kwa uchezaji wa mechi moja. Ana umri wa miaka 30 na bado ni mzuri, ni mpiganaji anayefurahisha katika uzito.

"Hakuna anayejali kuhusu akina Klitschkos."

Wakati huohuo, Schaefer, amesema Khan anaweza kujiandaa kupigana kwa ajili ya kutwangana na Floyd  Mayweather mwakani.

Bingwa wa mkanda wa WBA, Khan, ameanza maandalizi ya kucheza pambano la kuunganisha mataji dhidi ya Zab Judah mjini Las Vegas, Julai 23.

Pambano lake linalofuatia linaweza kuwa dhidi ya Erik Morales, Desemba na kisha kurejea Uingereza ambapo bondia huyo mwenye miaka 24, atahamia katika uzani wa welter na anaweza kutwangana na Kell Brook.

Huenda akatwanga na  Mayweather Novemba 2012.

Schaefer alisema: "Hii ni mipango mikubwa kwa Khan.

"Nimekuwa na mazungumzo na Mayweather na yuko tayari kutwangana na Amir."
 
Haye atakiwa Marekani
Friday, 08 July 2011 06:41
LOS ANGELES, Marekani

DAVID Haye, ameambiwa aende kupigana Marekani ili apate mafanikio kama bondia mwingine wa Uingereza, Amir Khan.Khan alikwenda kufanya mazoezi Marekani na akaja kuwa bingwa wa dunia baada ya kwenda Hollywood na kufanyishwa mazoezi na kocha mahiri wa Kimarekani, Freddie Roach.

Mtu maarufu katika ngumi, Richard Schaefer, anaamini kuwa kipaji cha Haye kinaweza kuzaliwa upya baada ya kupoteza pambano lake la uzito wa juu duniani kwa kupigwa kwa pointi dhidi ya Wladimir Klitschko, mjini Hamburg, Jumamosi usiku.

Haye sasa anataka kurudiana na Klitschko au kutwangana na kaka yake Vitali, ambaye ni bingwa wa mkanda wa WBC .

Lakini Schaeffer, ambaye ni Mtendaji Mkuu wa kampuni ya promosheni ya Oscar De La Hoya, Golden Boy, ambaye ni promota wa Khan na Haye alisema, "anatakiwa kuja na kupigana mapambano Marekani kwa mara ya kwanza.

"David hakuweza kucheza vizuri Jumamosi na sikufurahishwa na uchezaji wake.

"Lakini si sahihi kumjaji David kwa uchezaji wa mechi moja. Ana umri wa miaka 30 na bado ni mzuri, ni mpiganaji anayefurahisha katika uzito.

"Hakuna anayejali kuhusu akina Klitschkos."

Wakati huohuo, Schaefer, amesema Khan anaweza kujiandaa kupigana kwa ajili ya kutwangana na Floyd  Mayweather mwakani.

Bingwa wa mkanda wa WBA, Khan, ameanza maandalizi ya kucheza pambano la kuunganisha mataji dhidi ya Zab Judah mjini Las Vegas, Julai 23.

Pambano lake linalofuatia linaweza kuwa dhidi ya Erik Morales, Desemba na kisha kurejea Uingereza ambapo bondia huyo mwenye miaka 24, atahamia katika uzani wa welter na anaweza kutwangana na Kell Brook.

Huenda akatwanga na  Mayweather Novemba 2012.

Schaefer alisema: "Hii ni mipango mikubwa kwa Khan.

"Nimekuwa na mazungumzo na Mayweather na yuko tayari kutwangana na Amir."
 
DAVID Haye, ameambiwa aende kupigana Marekani ili apate mafanikio kama bondia mwingine wa Uingereza, Amir Khan.Khan alikwenda kufanya mazoezi Marekani na akaja kuwa bingwa wa dunia baada ya kwenda Hollywood na kufanyishwa mazoezi na kocha mahiri wa Kimarekani, Freddie Roach.

Mtu maarufu katika ngumi, Richard Schaefer, anaamini kuwa kipaji cha Haye kinaweza kuzaliwa upya baada ya kupoteza pambano lake la uzito wa juu duniani kwa kupigwa kwa pointi dhidi ya Wladimir Klitschko, mjini Hamburg, Jumamosi usiku.

Haye sasa anataka kurudiana na Klitschko au kutwangana na kaka yake Vitali, ambaye ni bingwa wa mkanda wa WBC .

Lakini Schaeffer, ambaye ni Mtendaji Mkuu wa kampuni ya promosheni ya Oscar De La Hoya, Golden Boy, ambaye ni promota wa Khan na Haye alisema, "anatakiwa kuja na kupigana mapambano Marekani kwa mara ya kwanza.

"David hakuweza kucheza vizuri Jumamosi na sikufurahishwa na uchezaji wake.

"Lakini si sahihi kumjaji David kwa uchezaji wa mechi moja. Ana umri wa miaka 30 na bado ni mzuri, ni mpiganaji anayefurahisha katika uzito.

"Hakuna anayejali kuhusu akina Klitschkos."

Wakati huohuo, Schaefer, amesema Khan anaweza kujiandaa kupigana kwa ajili ya kutwangana na Floyd  Mayweather mwakani.

Bingwa wa mkanda wa WBA, Khan, ameanza maandalizi ya kucheza pambano la kuunganisha mataji dhidi ya Zab Judah mjini Las Vegas, Julai 23.

Pambano lake linalofuatia linaweza kuwa dhidi ya Erik Morales, Desemba na kisha kurejea Uingereza ambapo bondia huyo mwenye miaka 24, atahamia katika uzani wa welter na anaweza kutwangana na Kell Brook.

Huenda akatwanga na  Mayweather Novemba 2012.

Schaefer alisema: "Hii ni mipango mikubwa kwa Khan.

"Nimekuwa nazungumza na myweather na yuko tayari kutwangana na Amir

Thursday, July 7, 2011

CCM Kuanza Kusherehekea Miaka 50 Ya Uhuru

 

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


Mwaka huu Sehemu ya nchi yetu, yaani Tanzania Bara itaadhimisha miaka hamsini ya Uhuru wake toka kwa Wakoloni. Uhuru huu uliopatikana miaka hamsini iliyopita ni kazi nzuri na ya Kizalendo iliyofanywa na Chama cha TANU.

Chama Cha Mapinduzi katika kukumbuka kazi hii nzuri ya kutafuta Uhuru wa nchi yetu kimeamua kufanya shughuli mbalimbali za kukumbuka kuzaliwa kwa chama kilicholeta Uhuru wa Tanzania Bara yaani TANU.

Itakumbukwa TANU ilizaliwa tarehe 7/7/1954 hapa Dar es salaam katika mtaa wa New street ambao kwa sasa unafahamika kama mtaa wa Lumumba mahali ambapo sasa ni  Ofisi Ndogo ya CCM Makao Makuu. Huo ukawa ndio mwanzo wa harakati za kudai Uhuru, Utu na Heshima ya Mwafrika katika nchi yetu.

Kwa kuienzi historia na kazi nzuri na ya Kizalendo iliyofanywa na TANU, Chama Cha Mapinduzi kimeamua katika kuadhimisha miaka hamsini ya Uhuru wa Tanzania Bara kuandaa shughuli mbalimbali za kijamii zikiwa na kauli mbiu Uhuru na Kazi, kauli maarufu katika miaka ya nyuma ambayo Baba wa Taifa Mwalimu J. K. Nyerere aliitoa katika hotuba yake ya kusisimua siku ya mkesha wa Uhuru wa Tanganyika mwaka 1961.

Mwalimu Nyerere aliitumia hotuba hiyo kuwaeleza wananchi wajiandae kuanza kufanya kazi kwa bidii ili kujiletea wao wenyewe na nchi maenedeleo. Maadhimisho haya yatafanyika nchi nzima kuanzia ngazi za matawi na kuwashirikisha wanachama wetu na wananchi wote kwa ujumla. Shughuli zitakazofanyika ni kama zifuatavyo:-

     i.        Usiku wa kuamkia tarehe 7/7/2011 Vijana wa CCM nchini watakutana maeneo mbalimbali kufanya shamrashamra za kuzaliwa TANU

    ii.        Tarehe 7/7/2011 asubuhi wanachama wa CCM na wananchi watakutana kwenye matawi yao na kufanya shughuli mbalimbali za kijamii kama vile, kufanya usafi, kusaidia ujenzi, kupanda miti, kutembelea wagonjwa mahospitalini n.k.

  iii.        Ikiwezekana kufanya matamasha mbali mbali yatakayowashirikisha vijana wasomi wanasiasa na wazee kujadili masuala mbali mbali yenye faida kwa Kata, Wilaya, Mkoa au Taifa kwa ujumla.

  iv.        Kufanya mikutano ya hadhara na kujikumbusha mafanikio yaliyopatikana kwa kila Mkoa na  Wilaya katika kipindi cha miaka 50 ya Uhuru.

Kwa Sehemu kubwa tunategemea walezi wa CCM wa Mikoa na Viongozi mbalimbali wa Kitaifa watashiriki shughuli hizo mikoani. Sherehe hizi zitaanza usiku wa tarehe 6/7/2011 kwa vijana wa CCM sehemu mbalimbali nchini kukutana na kusherehekea ikiwa ni pamoja na kufyatua MAFATAKI saa sita usiku ya siku hiyo, kama ishara ya kuzaliwa TANU.

Mwenyekiti wa CCM Taifa Dr. Jakaya M. Kikwete atashiriki sherehe hizi mkoani Dar es salaam, usiku wa Tarehe 06/07/2011 na tarehe 07/07/2011 asubuhi atakutana na Mabalozi wa Nyumba Kumi Mkoa wa Dar es salaam.

Ni mategemeo yangu vyombo vya habari vitashirikiana nasi katika kuuelimisha umma kuhusu historia hii muhimu ya Taifa letu na kutangaza matukio yote yatakayo ambatana na maadhimisho haya.

Wednesday, July 6, 2011

SIMBA YATINGA NUSU FAINALI KOMBE LA KAGAME

Wachezaji wa timu ya Simba wakishangilia baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Bunamwaya ya Uganda katika mchezo wa Robo Fainali Kombe la Kagame uliochezwa Julai 5,2011 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Kwa ushindi huo, sasa Simba imetangulia katika fainali hizo ambapo itamenyana na El Mereikh ya Sudan katika mechi ya nusu fainali mwishoni mwa wiki, ambapo El Mereikh ilikata tiketi hiyo baada kuifunga Ulinzi ya Kenya katika mchezo uliomalizika Julai 5,2011 kwa njia ya matuta

Saturday, July 2, 2011

Asema serikali imefanya maamuzi magumu



Mbunge wa Monduli (CCM), Edward Lowassa
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, amejibu hoja zilizotolewa na Mbunge wa Monduli (CCM), Edward Lowassa, wiki iliyopita kuwa serikali ya awamu ya nne imeshindwa kufanya maamuzi magumu, kwa kuorodhesha mambo mbalimbali ambayo yamesema ni magumu yakiwa yamechukuliwa na serikali.

 Pinda alisema hayo alipokuwa akijibu hoja za wabunge waliochangia mjadala wa bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka wa fedha wa 2011/2012, bungeni, mjini hapa jana jioni.  Lowassa akichangia mjadala wa bajeti hiyo wiki iliyopita, alisema kuna ugonjwa wa kuogopa kutoa maamuzi hivyo akataka serikali kutoa maamuzi na kusema: 

 “Heri ukosee kwenye kutoa maamuzi kuliko kutotoa maamuzi. Toeni maamuzi, acheni kuogopa, tumepewa nchi, tufanyeni maamuzi. Heri uhukumiwe kwa kutoa mamuzi kuliko kwa kutotoa maamuzi. Toeni maamuzi. Nasema tunaweza kufanya. Tukinuia, tukiamua, tunaweza kufanya.”

 Pinda alisema serikali ya awamu ya nne inayoongozwa na Rais Dk. Jakaya Kikwete ndiyo pekee imefanya maamuzi magumu na mazito kuliko serikali zote zilizopita.

 Alisema imekuwa ikifanya maamuzi thabiti na magumu, lakini kwa busara na tahadhari ili kutenda haki na kwa kuzingatia uwezo wake ili kulinda maslahi ya wananchi na kudumisha amani.

  Alisema katika kufanya maamuzi hayo, serikali imekuwa makini kuzingatia sheria, kanuni na taratibu.

 Aliyataja maamuzi magumu yaliyokwishafanywa na serikali ya awamu ya nne kuwa ni pamoja na kuwafikisha mahakamani waliokuwa mawaziri wa serikali zilizopita kutokana na tuhuma mbalimbali zinazowakabili za kutumia madaraka isivyo halali; na pia kujenga shule za sekondari za kata, ambazo zimewezesha wanafunzi wengi kupata elimu ya sekondari.

 Mengine ni kujenga Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom);  kujenga Chuo cha Serikali za Mitaa Hombolo; kukamilisha miradi yote 27 ya barabara kuu zilizoanzishwa na serikali ya awamu ya tatu; ujenzi na ukamilishaji wa miradi ya maji nchini; na kuwalinda watu wenye ulemavu wa ngozi (albino).

 Pia, kuondoa mpasuko wa kisiasa Zanzibar na kuanzisha serikali ya umoja wa kitaifa katika Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ); kupanua na kushamiri kwa demokrasia nchini kwa kiwango kikubwa; uhuru mkubwa wa vyombo vya habari; na kuruhusu kuanzisha mchakato wa kupata Katiba mpya. 

  “Lakini pia katika awamu hii ndipo tumefanya maamuzi mazito sana ya kuvunja Baraza la Mawaziri kufuatia kujiuzulu kwa aliyekuwa Waziri Mkuu, Mheshimiwa Edward Lowassa. Hili nalo halikuwa jambo jepesi hata kidogo. Inataka Moyo!” alisema Pinda.

Aliongeza: “... maisha ya serikali katika kutekeleza majukumu yake kwa dhana ya uwajibikaji wa pamoja kupitia Baraza la Mawaziri. Tunachohitaji ni kuvumiliana. Kuvuta subira, kwani mambo mema hayataki haraka!  Tutaamua na Tutafanya!”
 Akizungumzia suala la posho, alisema suala hilo ni muhimu kutazamwa kwa upana wake na kwa msingi ulioelezwa chini ya Mpango wa Miaka Mitano, yaani kuzungumzia posho zote.  

“Hii ni kwa sababu kwa mujibu wa Waraka wa Masharti ya Kazi za Mbunge; stahili za wabunge ni pamoja na zifuatazo: Mshahara wa mbunge kodi Sh. 588,000 ambao ulishakatwa, ambao haujakatwa kodi  ni Sh. 2,305,000, ukisakatwa kodi ni Sh. 1,717,000. Posho ya ubunge; posho ya vikao vya Bunge na kamati zake,” alisema Pinda.

  Aliongeza: “Posho ya madaraka kwa viongozi; Entertainment Allowance (posho za maburudisho) kwa viongozi; posho ya kujikimu ndani na nje ya nchi; posho ya mavazi anaposafiri nje ya Tanzania; posho ya msaidizi wa ofisi ya mbunge; posho ya usafiri wakati wa vikao vya kamati na mikutano ya Bunge; vilevile, kuna posho ya mafuta (Lita 1,000) kwa mwezi na Mfuko wa Maendeleo wa Jimbo (CDCF).”

 Pinda alisema kwa kuwa suala hilo lipo ndani ya Mpango wa Maendeleo, serikali italitafakari kwa undani na kuangalia posho zipi hazina tija na zipi zina tija na manufaa ya kuongeza ufanisi ili ikiwezekana zihuishwe na kujumuishwa ndani ya mishahara au vinginevyo kama itakavyoonekana inafaa.

 Alisema serikali pia itaangalia suala la kupunguza gharama za matumizi ya serikali kwa ujumla wake ikijumuisha kupunguza matumizi yasiyo ya lazima katika taasisi zote za serikali.

  Pinda alisema kwa maelekezo ya Rais Kikwete, uamuzi wa kuhamia Dodoma hauna budi kutekelezwa na kusisitiza kuwa hata kama fedha zimetengwa, Ofisi ya Waziri Mkuu itajengwa Dodoma.

Friday, July 1, 2011

Tanzania kuanza kuchimba madini ya Urani

Duma
Duma wa Selou
Tanzania itaanza kuchimba madini ya urani katika mbuga ya wanyama ya Selous, eneo lililo chini ya udhamini wa shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughilikia mazingira maarufu kama World Heritage.
Akizungumza na Idd Seif wa Idhaa ya kiswahili ya BBC, Waziri wa maliasili na utali iwa Tanzania, Ezekiel Maige, alisema kuwa sehemu wanayohitaji kutumia kwa kuchimbia mgodi wa urani ni 0.69%,
hivyo kupunguza eneo la mbuga ya wanyama kwa chini ya 1%.
Kwa mujibu wa Waziri Maige, WHC imesema itatoa kibali iwapo tu masharti ya kutunza mazingira yatakuwa yamezingatiwa. Fedha zitakazopatikana kutokana na madini hayo zitasaidia kutunza
mbuga hiyo alisema Maige.
Kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la Utamaduni UNESCO, hekta milioni tano la hifadhi ya mbuga ya Selou ina idadi kubwa ya Tembo, vifaru weusi, Chita, viboko na mamba na haijaharibu na
shughuli zozote za kibinadamu.
Katika mahojiano na Idhaa ya Kiswahili ya BBC, Bw Maige alisema mradi huo bado uko katika hatua za mwanzo lakini utaathiri kwa asilimia 0.69 tu ya mbuga ya sasa na utakuwa ni chanzo muhimu
cha mapato ya nchi.
Makampuni yanatarajia kupata $200 milioni kwa mwaka kutokana na uchimbaji wa Urani na kati ya hizo $5 milioni zitalipwa kwa serikali ya Tanzania, alisema.
Sehemu ya mapato hayo itasaidia kutunza mbuga hiyo na mradi utatoa ajira kwa watanzania 1,600.
Katika mkutano wa mwaka wa kamati ya WHC, waziri Maige alisema, kulikuwa pia na wasiwasi kuhusu Msitu wa hifadhiwa Undendeule ulio kusini mwa mbuga ya Selou.
Lakini Bw Maige ambaye pia anashughulikia Utalii alisisitiza kuwa hakutakuwa na mathara kwenye msitu huo wa hifadhi ambao kwa sasa unaigharimu serikali $490,000 kwa mwaka kuutunza. Na
mapato yatakayotokana na uchimbaji wa madini hayo utasaidia kulipa askari wanaodhibiti ujangili.
Alisema Tanzania haikuhitaji kibali kutoka UNESCO ili kuendelea na mpango wake wa kuchimba Urani, lakini mataifa ya Afrika Mashariki yalitaka kujiridhisha na mapendekezo ya shirika hilo.
"mradi huu wa Urani utaanza," aliiambia BBC.
Aliongeza kuwa WHC Tanzania ifanye tathmini yenyewe itakayopitishwa na Tume ya Mazingira ya nchi hiyo.
Hatua ya pili ilikuwa ni hitaji la ujumbe wa wataalam kutoka UN kutembelea aeneo hilo na kutoa mapendekezo yake kuhusu kulinda na kutunza mfumo wa ekolojia.
Waziri alisema baada ya uamuzi huu taarifa itapelekwa katika mkutano mwingine wa WHC mwakani kuhusu mipaka ya Mbuga ya Hifadhi ya Selou.
Bw Maige aliongeza kuwa utafiti unaonyesha kuwa hakuna haja ya kuwa na wasiwasi kuhusu sumu ya mionzi inayotokana na uchimbaji wa Urani katika eneo hilo.
"Kiwango cha mionzi kitabakia kuwa kile kile, haitakuwa na hatari kwa binadamu," alisema.

Strauss-Khan aachiwa bila dhamana

Aliyekuwa mkuu wa shirika la fedha duniani, IMF Dominique Strauss-Khan ameachiwa huru baada ya kupewa kifungo cha nyumbani na kurejeshewa dhamana yake ya dola za kimarekani milioni 3.7.
Imeripotiwa waendesha mashtaka wamekubaliana kuwa Bw Strauss-Khan aachiliwe huru "kwa udhamini wake mwenyewe," ikimaanisha aahidi kufika mahakamani.
Anatuhumiwa kumdhalilisha kijinsia mhudumu kwenye hoteli moja mjini New York mwezi Mei 14.
Bw Strauss-Khan na mkewe

Lakini kesi hiyo inakaribia kufutwa baada ya kuibuka mashaka makubwa juu ya uaminifu wa aliyemshtaki.
Mwanasiasa huyo wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 62 - aliyeonekana kuwa miongoni mwa wagombea wa urais wanaoongoza- alifika mahakamani siku ya Ijumaa.
Baada ya kutathmini taarifa za mwendesha mashtaka kutoka kwenye ofisi ya mahakama ya wilaya ya Manhattan, jaji ametangua masharti makali ya dhamana aliyopewa na Bw Staruss-Khan, lakini aliamuru kushikiliwa kwa hati yake ya kusafiria ili asiweze kusafiri nje ya Marekani.
Miongoni mwa yaliyowasilishwa ni taarifa kuwa mhudumu huyo alitoa ushahidi usio wa kweli kwa wazee wa baraza, bila kusema alisafisha chumba chengine kabla ya kumwambia msimamizi wake juu ya madai ya kudhalilishwa kijinsia.

BARACK OBAMA NA MATUMAINI FEKI YA WAAFRIKA NA WEUSI

 
Mapema mwezi wa Juni, tarehe 3 mwaka huu, Barack Obama alifikia hatua kubwa katika harakati zake za kuteuliwa mgombea wa Chama cha Democratic. Ni hatua ambayo Wamarekani wanaiita (Nominee designate) mgombea mtarajiwa. Siku hiyo hapa Tanzania mkutano wa nane wa Taasisi ya Sullivan ulikuwa ukifanyika. Aliyewahi kujaribu harakati za kuchaguliwa, Mchungaji Jesse Jackson alinena kwa furaha akijivunia ni ushindi kwa weusi. Karibu waongeaji wote walizungumza juu ya hili kwa maono ya ushindi wa weusi.
Nikiwa kama mtanzania, mtu mweusi, nimefarijika pia kwa ushindi wa Seneta Barack Obama. Kufarijika kwangu si kwa mashiko ya rangi; yaani mweusi kashinda basi nami nifurahi. Kwangu nimeshangazwa karibu weusi wote wanamshabikia Obama eti kwa kuwa ni mweusi. Nina mashaka kama kweli hisia zetu zinaegemea zaidi rangi basi nadiriki kusema kuwa tusipokuwa makini nasi pia ni wabaguzi wa rangi wakubwa.
Nina wasiwasi: wote wanaouchukulia ushindi wa Obama kama ushindi kwasababu ni mweusi basi wamepotea njia. Ni lazima watu tufikiri kwa kina na si kushabikia tu ilihali inawezekana kabisa Obama hatakuwa na maslahi yoyote kwa waafrika na hata kwa watu weusi sehemu mbalimbali za dunia.

Labda niwarejeshe kwenye historia: Raisi wa zamani wa Marekani, Ruthirford Hayes aliwahi kunena kuwa “Us government is a government of the corporations, by corporations for the corporations”. Alimaanisha kuwa serikali ya Marekani ni serikali ya Makampuni, kwa maslahi ya Makampuni na inaendeshwa na Makampuni. Hapa alikuwa anajaribu kutanzua kiza kinene (illusion) kwenye maana ya demokrasia kama ilivyokuwa imeelezwa awali na mtangulizi wake Lincoln pale alipoweka maneno: “Government of the People for the People by the People” yaani: “serikali ya watu, kwa watu na maslahi yao” katika katiba ya nchi hiyo.

Ni katika msingi wa kuingalia serikali ya Marekani kama inayoongozwa na mtizamo wa Katiba kuheshimiwa bila ubazazi wa aina yeyote kama tunavyoshuhudia hapa kwetu, basi kama Obama atachaguliwa kuwa raisi wa Marekani tujue kabisa atafanya kazi kwa misingi ya Rais wa zamani Ruthirford Hayes. Hapa ndipo panaponifanya nisiwe na matumaini kama kweli mtu mweusi kuwa Rais wa Marekani basi tutafaidika na lolote tofauti na marasi wengine weupe waliokwishapita na kutawala Marekani. Ni vyema tumfurahie Seneta Obama kutokana na wajihi wake: ni jinsi gani ameweza kuchambua masuala mbalimbali kwa ufasaha na kuonesha jinsi gani anavyoweza kufikiri. Ni kigezo hiki tu naweza kufurahia ushindi wa Obama na wala kamwe si rangi yake. Kinyume na hapo naona ni mtizamo wa kibaguzi ambao hauna nafasi katika dunia ya kileo.

USHINDI HARAKATI ZA MTU MWEUSI

Kuna wengine wanauona ushindi wa Seneta Obama kama vile ni ushindi wa harakati za kutafuta haki za mtu mweusi. Hebu nikumbushie harakati za kumkomboa mtu mweusi nadhani zilianza siku nyingi chini ya watu kama akina Willium Du Bois, Marcus Garvey, George Padmore, Malcolm X, Martin Luther King, Nelson Mandela, Julius Nyerere, Jomo Kenyatta, Kenneth Kaunda, Robert Nesta Marley hadi akina Jesse Jackson na Luis Farhani wa leo hii Marekani.

Nimejaribu kupiga picha na nimeona hadi leo hii mtu mweusi kafikia mafanikio mengi katika nyanja nyingi. Kwa mfano, miongo mitatu iliyopita tunaweza kung’amua mafanikio ya mtu mweusi kama ifuatavyo:
Mosi, mwishoni mwa miaka ya 1970, waafrika weusi wa Marekani waliweza kutawala fani ya muziki kimataifa pale mziki aina ya kufokafoka ulikuwa sana kuanzia New York na kuua kabisa muziki wa Rock uliokuwa ukitawala.
Pili, baada ya mafanikio ya muziki, mwafrika asilia alianza kuonesha mafanikio duniani katika mchezo wa soka. Mwaka 1990, timu ya Taifa ya soka ya Cameroon (Indomitable Lions) ilifikia hatua ya robo fainali ya Kombe la dunia kule Italia chini ya Roger Milla. Baadaye mwaka 2002 kule Korea na Japan timu nyingine ya Senegal nayo ilifika hatua kama hiyo.

Jambo la tatu, katika miaka hiyo hiyo ya 1990, kule Afrika ya Kusini, Nelson Mandela na wafungwa wenzake kama akina Govan Mbeki, Walter Sisulu waliachiwa huru. Baadaye mwaka 1994 waafrika walio wengi wakafanikiwa kuunda serikali ndani ya nchi ambayo walinyimwa haki hiyo kwa miongo kadhaa. Si hapa Afrika tu mtu mweusi kafanikiwa, kwa mfano, mwaka 1997, kijana mweusi wa Marekani: Eldrick ‘Tiger’ Woods akaweka historia kushinda mashindano makubwa ya mchezo wa gofu “US Masters” na ametawala mchezo huo kidunia hadi ninapoandika makala hii. Mchezo wa kikapu ndio usiseme, mtu mweusi katawala hasa.

TIJA YA MAFANIKIO YA MTU MWEUSI

Kwa ujumla mtu mweusi kafanikiwa sana kwa miaka ishirini iliyopita si kwenye fani ya sanaa na michezo tu. Bali hata kwenye mambo ya uongozi wa taasisi nyeti za kimataifa, mwafrika tayari anajivunia kuweza kuongoza katika nyadhifa za juu kabisa. Kwa mfano, Umoja wa Mataifa (UN) , mwaka 1991 – 1994 ulikuwa chini ya Butros Butros Ghali raia wa Misri, baadaye akarithiwa na mweusi hasa Koffi Atta Annan wa Ghana mwaka 1995. Ni kipindi hichohicho, Jumuiya ya Madola ilikuwa chini ya Chief Emeka Anyaoku wa Nigeria kama Katibu Mkuu. Haya yote ilikuwa ni kuionesha dunia kuwa mtu mweusi anaweza na anatambulika. Lakini tujiulize: Je kulikuwa na msaada gani mkubwa kwa waafrika pale yote haya yalipojitokeza? Nakumbuka tulifurahi na kushangilia kutokana na hisia zenye mashiko ya rangi.

Watu wengine wanaweza kujiuliza labda mafanikio mengi ya mtu mweusi niliyoyaelezea hayakutokea Marekani bali hapa Afrika chini ya waafrika. Lakini kwa sasa yanatokea kule Marekani, ambalo ndilo Taifa linalotoa mwongozo wa dunia basi hatuna budi kuwa na matarajio. Na hii ndio hisia ninayoiona miongoni mwetu wengi kama “matumaini feki”. Kwangu siamini hivyo na kamwe sitaamini. Labda nikumbushie tu pale Raisi George Bush alipoingia madarakani na kumteua Collin Luther Powel kama mweusi wa kwanza kuwa Waziri wa Mambo ya Nje, yaani cheo cha juu kabisa baada ya Raisi na Makamu wake Marekani. Raisi Bush alimteua baadaye mweusi mwingine Condoleza Rice katika nafasi hiyo ya juu kabisa hadi wakati naandaa makala hii.
Pia ni miaka si chini ya mitatu iliyopita, mwafrika mzaliwa wa Uganda John Sentamu alichaguliwa kuwa Askofu wa jimbo la York huko Uingereza. Hii ni nafasi ya pili kwa cheo ndani ya kanisa la Anglikana duniani. Katika haya yote yanayohusu ukombozi wa mwafrika ni mafanikio ambayo wanaharakati wanatumia mara nyingi neno la kiingereza “African Renaissance” yaani kuzaliwa upya kwa mwafrika.
Kwangu hili naliona pia kwa mtizamo huo kwani mwafrika ameweza kuondokana na kadhia za kibaguzi za zamani. Lakini tujiulize swali: Hivi mafanikio yote hayo yamesaidiaje weusi wa dunia hii? Tuache ukichaa, hebu angalia hata kule Afrika ya Kusini sasa mtu mweusi anapinga mweusi mwenzake kuishi nchini mwake. Umasikini wa mtu mweusi uliosababishwa na ufisadi wa wanaharakati wa zamani umetufikisha hapa tulipo. African Reinassance imepoteza mwelekeo huko Afrika Kusini kwa Madiba. Yote ni kwasababu mtu mweusi amekubali awe mtumishi na wakala wa mfumo wa kiutawala wa aina ya: “ corporate by corporation for the corporation”. Akina Raisi Mbeki na wapigania uhuru wenzake wamegeuka umma wa weusi na kuacha kuwatumikia na kuyatumikia makampuni.

Vivyo hivyo, nadhani hata Seneta Barack Obama atafuata mwelekeo huohuo kwa kuitumikia katiba ya Marekani ambayo imejaa lugha ya giza ikimaanisha mambo ambayo kimatendo ni kinyume na maneno. Yaani ikifuata mwelekeo wa Raisi Hayes badala ya ule sahihi wa Lincoln.
Ndio maana nilishangazwa sana mara baada ya Obama kuthibitisha kuwa ni mgombea mtarajiwa, hotuba yake ya kwanza mjini Washington ilikuwa ni mbele ya umati wa watu 7000 uliojumuisha “Kamati ya Mambo ya Waisraiel – Wamarekani ( Jewish American Israel Public Affairs Committee – AIPAC. Tujiulize ikiwa weusi wengi ndio waliompigia kura ilikuwaje aanze na shukrani kwa Wayahudi?

Dhahiri mwelekeo hapa wa dunia lazima tutumie bongo kufikiri na si kufuata hisia tu. Barack Obama hana njia nyingine ila ataungana na wale wengine niliowataja awali kama alama ya “African Reinassance” ambao wamemtangulia katika kuwatumikia wazungu. Kwani katika demokrasia ya leo, ule mtizamo wa Raisi Lincoln ndivyo sivyo. Mambo ya ‘Serikali ya watu, kwa watu na maslahi yao’ ni hadithi ya alinacha. Democrasia leo ni kutumikia makampuni makubwa yenye ushawishi. Haya ndiyo yenye kupenyeza rupia kusaidia kampeni za akina Seneta Obama ili wayatumikie pindi watakaposhinda. Ni kama vile hapa kwetu Tanzania vigogo fulani walivyojiundia vikampuni kwa mgongo wa EPA ili kupata fedha za kampeni. Obama yeye hakutumia mbinu za kibazazi za kujiundia vijikampuni feki ila anafadhiliwa na makampuni ambayo lazima alipe fadhila.

Mwisho, Seneta Obama ataungana na waliomtangulia: Koffi Annan, Colin Powel, Condoleza Rice, Chief Emeka Anyaoku na hata mama yetu mpendwa Asha Rose Migiro ambao walitumika na wengine wanatumika kwa sasa kama kielelezo feki cha kioo cha ubinadamu wa serikali za Marekani na Ulaya kukubalika ulimwenguni mbele ya umma wa watu weusi. Kwa mtizamo wangu huu ni lazima wale wote wenye mawazo kuwa Obama atasaidia weusi na hasa sisi waafrika waandike maumivu na masikitiko. Kwani akishakuwa Rais, kipaumbele kitakuwa ni maslahi ya Marekani kwanza kwa kufuata maneno ya Raisi Rutherford Hayes. Yaani kutumikia makampuni mbalimbali kabla ya kutumikia wapiga kura. Je tutarajie kama Raisi wa Marekani hatumikii watu wake, je atatumikia watu walio mbali naye kama sisi waafrika? Tuache ubaguzi tufikiri sana na tuangalie kwa bongo zetu na si kwa mioyo.

KUMBUKUMBU YA DKT MARTIN LUTHER KING JR NA TAFAKURI KUHUSU "I HAVE A DREAM" YA NYERERE (MAKALA KATKA GAZETI LA "MTANZANIA" LA LEO

Powered by Translate


Siku chache zilizopita Wamarekani waliadhimisha siku ya Dakta Martin Luther King Jr,mmoja wa wapigania haki za Waamerika Weusi.Historia inamkumbuka Dkt King (aliyezaliwa mwaka 1929 na kuuawa kwa risasi mwaka 1968)kama nguzo muhimu katika kupigania haki za Waamerika Weusi nchini humo.Pengine kilichomfanya wanaharakati huyo akubalike zaidi ni imani yake ya kudai haki kwa njia za amani.

Miaka mitano kabla ya kuuawa,mwaka 1963,Dkt King alitoa hotuba ambayo hadi leo imeendelea kuwa na mvuto mkubwa sio nchini Marekani pekee bali pia sehemu mbalimbali duniani katika mapambano ya kudai usawa.Katika hotuba hiyo iliyopewa jina “I Have a Dream” (“Nina Ndoto”,kwa tafsiri isiyo rasmi),Dkt King alieleza matamanio yake kuona Waamerika Weusi na Weupe wakiishi pamoja kwa amani na usawa.Hotuba hiyo iliyotolewa mbele ya watu zaidi ya laki mbili,inakubalika miongoni mwa wengi kama moja ya hotuba za muhimu kabisa katika historia ya Marekani.Mwaka 1999,hotuba hiyo ilichaguliwa na wasomi kuwa ni hotuba bora kabisa za karne ya 20.

Miongoni mwa nukuu muhimu katika hotuba hiyo ni pamoja na (kwa tafsiri yangu isiyo rasmi) “…nina ndoto kwamba siku moja taifa hili litasimama na kuishi kama inavyotamkwa kwenye imani yake….nina ndoto kwamba siku moja watoto wangu wanne wataishi katika taifa ambalo hawatahukumiwa kutokana na rangi ya ngozi zao bali tabia/utu wao….nina ndoto kwamba siku moja watoto wa waliokuwa watumwa na watoto wa waliokuwa wamiliki watumwa watakaa pamoja katika meza ya undugu…”

Msukumo uliotokana na uongozi wa harakati za Dkt King ulisaidia sana kubadili historia ya Marekani hususan usawa kwa (Wamarekani) Weusi, na kupelekea mabadiliko mbalimbali dhidi ya sheria za kibaguzi.Miongoni mwa sheria hizo ni pamoja na “Civil Rights Act” ya mwaka 1964 iliyoharamisha ubaguzi kwenye sehemu mbalimbali katika jamii.Mwaka uliofuata, “Voting Rights Act” ilipitishwa na kufuta kipengere kilicholazimisha wapiga kura watarajiwa kufanya testi za kupima uwezo wa kusoma na kuandika (wengi wa waathirika wa kipengere hicho walikuwa Wamarekani Weusi ambao walikuwa na maendeleo duni kielimu kutokana na kubaguliwa).

Maadhimisho ya siku ya Dkt King yamekuwa yakitoa changamoto nzuri kwa jamii ya Wamarekani kutafakari mahusiano kati ya Weupe na Weusi.Wengi hujiuliza iwapo ndoto za Dkt King zimetimia kweli,zinaelekea kutimia au hazina dalili ya kutimia kabisa.Ni maswali magumu ambayo yanahitaji uchambuzi wa kina kuyajibu,na pengine hata kwa uchambuzi wa kina bado inaweza kuwa vigumu kupata jawabu moja linalokubalika.Kingine kinacholeta ugumu wa kupata jawabu ni tofauti ya vizazi.Kwa walioishi nyakati za ubaguzi wa rangi na kushuhudia harakati za Dkt King wanaweza kuwa na mtizamo tofauti kuhusu kutimia kwa ndoto za mwanaharakati huyo ukilinganisha na kizazi cha hivi karibuni ambacho kinamwelewa Dkt King kupitia kumbukumbu za historia tu.

Hata hivyo ni rahisi kukubaliana kwamba harakati za Dkt King na wenzie zimesaidia kuleta mabadiliko makubwa ikiwa ni pamoja na hayo ya kisheria niliyotaja awali.Wapo wanaokwenda mbali zaidi na kutoa mifano ya mafanikio ya Waamerika Weusi maarufu kama Jenerali Colin Powell na Condoleeza Rice ambao wameshika nafasi nyeti katika uongozi wa taifa hilo.Lakini mfano mzuri zaidi ni Barack Obama,seneta Mweusi anayewania kuteuliwa kugombea urais wa nchi hiyo kupitia chama cha Democrats.Akiteuliwa kuwa mgombea,ataweka historia ya pekee nchini humo,na akifanikiwa kushinda urais basi hiyo itakuwa zaidi ya kuweka historia (tuite kuandika historia upya).Hata kama atashindwa,mafaniko aliyokwishafikia hadi sasa ni hatua muhimu katika kutimia kwa ndoto za Dkt King.

Afrika nayo imetoa akina Dkt King kadhaa,na kwetu Tanzania tunajivunia Baba wa Taifa marehemu Julius Nyerere ambaye (kama Dkt King) alikuwa na ndoto zake kadhaa ambazo kimsingi zilihusu kuwa jamii yenye usawa.Ndoto za Mwalimu zilivuka mipaka ya Tanzania kuhakikisha kuwa Afrika yote inakuwa huru.Mchango wa Mwalimu katika mapambano ya ukombozi kusini mwa Afrika utaendelea kukumbukwa milele.Na pengine hapo ndipo baadhi yetu tunagundua mabadiliko ya vizazi yanavyochangia kusahaulisha historia.

Mara nyingi napokutana na vijana Waafrika wenzangu (wanaoishi hapa Uingereza) kutoka nchi kama Zimbabwe,Zambia,Angola,Msumbiji,Afrika Kusini,Namibia na Uganda,nabaini kwamba wengi wao aidha wamesahau au wanapuuza mchango wetu katika ukombozi wa nchi zao (kwa Uganda ni kumng’oa Nduli Idi Amini).Angalau Wazimbabwe wanaweza kuwa na kisingizio kwamba kutokana na ubabe wa Mugabe,baadhi yao wanaweza kutoona faida ya kumkimbiza mkoloni na kujipatia uhuru.

Lakini pengine si busara sana kuwalaumu wanaopuuza mchango wa Mwalimu na Tanzania kwa ujumla katika ukombozi wa nchi zao kwani inawezekana kabisa wanafuatilia kinachoendelea nchini mwetu na kugundua kwamba baadhi yetu tumetupilia mbali kabisa jitihada za Baba wa Taifa kuhakikisha tunajenga jamii yenye usawa.Kwa vile dunia ni kama kijiji,katika zama hizi za utandawazi,majirani zetu hao watakuwa wanasoma na kusikia habari kuhusu ufisadi nchi mwetu,na pengine kubaki wanajiuliza “hivi hawa si ndio waliokuwa wanapigania usawa barani Afrika?Mbona wenyewe wako sasa wanafanyiana hivi?”.

Mwalimu alifariki huku baadhi ya ndoto zake zikiwa hazijatimia.Wachambuzi wazuri wa siasa wanadai kwamba baadhi ya ndoto hizo zilishindikana hata kabla hajang’atuka (kwa mfano upinzani wake wa awali dhidi ya ushirikiano na mashirika ya fedha ya kimataifa).Lakini nadhani Mwalimu aliumia zaidi kuona Azimio la Arusha likizikwa hai na Azimio “la kimyakimya” la Zanzibar (naliita hivyo kwani sijawahi kuona “document” yoyote rasmi inayoelezea kilichomo kwenye Azimio hilo).

Wakati Dkt King anaweza kufarijika huko aliko iwapo angeweza kufahamu baadhi ya mambo yanayoendelea sasa nchini Marekani (hususan kuhusu Obama) nashindwa kuhisi ni lipi litakalokuwa linampa furaha Mwalimu huko aliko tukiweka pembeni suala la amani na utulivu.Na hata katika hilo (la amani na utulivu) wapo wanaodai kuwa ni ya kufikirika zaidi kwani ni ukweli usiopingika kwamba masikini ni wengi zaidi kuliko matajiri,na yayumkinika kusema kwamba matumbo ya masikini hao hayana amani wala utulivu.

Kadhalika,kuna wanaodai kwamba kigezo cha amani na utulivu kimekuwa kikitumiwa vizuri zaidi na mafisadi wanaoamini kwamba Watanzania ni wapole sana na hawako tayari kuchezea lulu ya amani na utulivu kwa vile tu flani kakwiba mabilioni ya umma.Pengine mafisadi hao wako sahihi kwani tumekuwa tukishuhudia baadhi ya watu wakiua,wakapewa dhamana za chapchap na kuendela na maisha yao kama kawaida huku hatima ya kesi zao ikisubiri isahaulike akilini mwa watu.Wakati hayo yakitokea,magereza yetu yamejaa wamachinga wanaotafuta ridhiki mitaani na wafungwa wengine ambao inawezekana kabisa walijiingiza kwenye wizi wa nyanya au kuku kwa vile tu hawakuwa na njia nyingine ya kujipatia kipato.Uhalifu ni uhalifu,na kila mhalifu anastahili adhabu lakini inatatiza kuona wahalifu wengine wakiendelea kula raha kana kwamba waliyofanya si kinyume cha sheria.

Tofauti kubwa kati ya ndoto ya Dkt King na Mwalimu ni kwamba wakati Wamarekani Weusi wanafanya kila jitihada kuenzi jitihada za Dkt King kwa kuendeleza mapambano dhidi ya ubaguzi na kupigania usawa,sie tuko kwenye mgawanyiko mkubwa kati ya wachache walionacho wasiosubiri kuongezewa bali wanapora, na wengi wasio nacho ambao hata kile kidogo walicho nacho kinaporwa.Hili ndio tishio kubwa,sio tu kwa ndoto za Mwalimu,bali hata kwa hiyo lulu yetu ya amani na utulivu.

Thursday, June 30, 2011

TUZUNGUMZE MAPENZI!

 

Kila mtu anajua habari za mapenzi,hata wewe unayesoma habari hii unajua habari hizi. Mapenzi ni matunda matamu na pia ni matunda machungu.Sijui inategemea nini lakini nadhani ni kadri unavyoyapata,unavyoyala,na unavyojisikia wakati unaanza kula au unapomaliza.
Blog hii ni ya watu wazima,watu wanaojua nini maana ya mapenzi au wanaojaribu kujua zaidi.Nimeamua kuanzisha blogu hii kwa sababu najua ipo haja ya watu kuendelea kubadilishana mawazo juu ya mapenzi,ngono na mengineyo yanayohusiana na miili yetu,zikiwemo afya zetu.Si mnajua kwamba kitumbua siku hizi kimeingia mchanga ndugu zangu?

Kwa hiyo keti kitako tuanze kuyachambua masuala ya mapenzi. Kwa utaalamu wangu wa masuala haya nadhani nitakuwa tayari kujibu maswali yenu,hoja zenu nk kuhusiana na mapenzi,kujamiiana(ngono) na mengi mengineyo. Jisikie huru kunitumia email au kuuliza swali lako hapa hapa,nitakujibu. Lakini kwa kuanzisha hoja,hebu niambie,mapenzi ni nini kwa jinsi unavyoelewa wewe?Ni kwanini eti watu wanauana,wanafarakana,wanachinjana,nchi zinaingia kwenye vita kisa mapenzi? Je hayo yanabakia kuwa mapenzi au chuki? Kuna uhusiano gani kati ya mapenzi na wivu?Yupi ana nguvu kumshinda mwenzake?

WANAWAKE NA PESA


Msomaji mmoja wa blog hii kuhusu mapenzi (hakupenda kuweka jina lake) amekuwa wa kwanza kuuliza swali.Nitaliweka swali lake kwa kutumia italics likifuatiwa na jibu langu. Nitakuwa najaribu kuyaweka majibu yangu kwa ufupi sana(not in details) ili kuokoa nafasi na pia muda wako. Hata hivyo,tunaweza kuwasiliana kwa email kama utahitaji details zaidi na pia michango,mawazo,maoni nk yanakaribishwa sehemu ya mbele ya maoni.

SWALI:Sasa mimi nauliza kwa nini wasichana wengi wanapenda wanaume wenye pesa hata kama wana uwezo wa kupata pesa pia.Kwa nini wasijiamini nao kama wanaume na kufikiria kuwa pesa siyo jambo la maana sana kama unampenda mwenzio?

JIBU:Swali hili lina historia ndefu sana na ya aina yake. Ni swali lenye umri mkubwa pengine kama ilivyo dunia yetu. Ni swali zuri sana. Mara nyingi limeulizwa kwamba hivi mwanamke anataka nini zaidi,pesa,ulinzi au mapenzi na mapenzi motomoto kitandani?(Wenzetu wazungu lugha yao inaweza kutenganisha dhana hizi mbili kirahisi zaidi;love or good sex) Kwa bahati mbaya hata wanawake wenyewe wamejikuta kila mara wakipambanua mambo yote haya kwa sababu kwanza wanaume wenye sifa zote hizo hapo juu kwa pamoja ni kama hawapo na dunia imebadilika na inaendelea kubadilika.

Kabla sijaendelea mbele naomba ieleweke kwamba sio kila mwanamke anaweka pesa mbele na sio kila mwanamke duniani bado anaamini kwamb a yeye ni mtu wa kupokea,kuhudumiwa na kutunzwa tu.. Hali ni tofauti baina ya sehemu na sehemu,nchi na nchi,bara na bara,tamaduni na tamaduni. Kwa mfano hapa ninapoishi tamaa ya wanawake kupenda na kuthamini pesa inazidi kupungua kadri siku zinavyokwenda. Siku hizi wanawake nao wapo mstari wa mbele kuchangia kwa njia zote zinazowezekana kuboresha maisha na kwa maana hii mapenzi.

Sifa zinaenda kwa wale wanawake wanaojulikana kama “feminists” ambao kwa namna moja au nyingine wanachojaribu kufanya ni kumkomboa mwanamke kutoka kwenye fikra za yeye kuwa chombo cha kupokea tu bila kushiriki kwenye kutafuta na kutoa.

Pamoja na juhudi za dhati za wanasaikolojia katika kubadili muelekeo wa fikra za wale wanawake wanaothamini pesa na kubakia wakidhani kwamba jukumu la kutoa pesa,kuchangia matumizi,kuthamini mapenzi zaidi haliwahusu,bado wapo wengi wenye msimamo tofauti.Wao bado wamegubikwa na utando wa historia,utando wa saikolojia na pia utando wa nafasi ya mwanaume dhidi ya mwanamke au dhidi ya jamii inayomzunguka.

Msimamo wao ndio muuliza swali wetu, anaouwekea msisitizo;kwamba kwanini hata wale walio na hali nzuri kifedha bado wanadhani sio jukumu lao kusaidia,kuchangia katika matumizi?

Sababu kubwa,kama nilivyoanza kuanisha hapo juu ni fikra. Kihistoria,tangu mwanzo wa dunia hii mwanaume amekuwa mtafutaji na mwanamke akabakia nyumbani kulea watoto,kutunza kaya na kuhakikisha kwamba familia inakuwa bora. Katika nchi zetu za kiafrika,kwa mfano,utaratibu ukawa binti akue,akishavunja ungo basi aoelewe akaanzishe familia yake.Wazo la yeye kuandaliwa kama mtafutaji halikuwepo kabisa. Kwa bahati mbaya dunia tunayoishi hivi leo inatoa nafasi kidogo sana kwa ustawi wa taratibu kama hizo.Lakini je,fikra au utaratibu huo umetokomea vichwani mwa watu,hususani wanawake wenyewe? Jibu rahisi ni kwamba bado fikra ile ya mapokeo ipo miongoni mwa wanawake wengi.

Sababu ya pili ni ya asili kimaumbile na kisaikolojia vile vile. Kimaumbile mwanaume ameumbwa awe mkakamavu zaidi,awe mlinzi wa mwanamke.Ingawa siku hizi mambo yanazidi kubadilika ambapo utaona wanawake wengi katika shughuli ambazo hapo zamani zilidhaniwa kuwa za wanaume peke yao,bado kwa kiwango kikubwa, hali imebakia kama ilivyokuwa enzi za Adam na Hawa. Sasa “protection” hii haishii kwenye ulinzi wa kimaumbile tu kwamba nyumba ikivamiwa mwanaume ndiye anategemewa zaidi kuongoza mapambano dhidi ya wavamizi,bali huenda pia hata kwenye financial protectionism ambapo bila kujali mwanaume ana kiasi gani cha fedha,bado anategemewa kuwa mtoaji.

Mwishoni nashauri pia tusisahau watu wanaoitwa “sugar mummies”. Hawa pia ni wanawake ambao msimamo wao ni tofauti kabisa na wanawake wengi ingawa motives zao ni tofauti na mara nyingi zinaeleweka.Pengine siku moja tutapata nafasi ya kuzungumzia saikolojia zao pia.

KIDOKEZO: Hivi unafahamu kwamba mfalme wa Morocco wa karne ya 16 (Moulay Ismail) alikuwa na watoto wanaokadiria kufikia 1,042?

Zikowapi Tafiti za Muziki wa Kizazi Kipya - Fid Q



Msanii wa muziki wa kizazi kipya anayetamba katika miondoko ya Hiphop,Fareed Kubanda aka Fid Q ametoa wito kwa wadau wa sanaa hasa waandishi kujikita katika kuandaa machapisho na vitabu vinavyoelezea undani wa muziki huo.

Wito huo umekuja wakati ambao hakuna tafiti zinazofanywa katika muziki huo hapa nchini kiasi cha kutokuwepo kwa historia ya moja kwa moja inayoeleza asili ya muziki huo na nini hasa kilitokea hadi vijana wengi kujikita katika muziki huo ambao kwa sasa umepata umaarufu mkubwa.

Akizungumza kwenye Jukwaa la Sanaa wiki hii,Fid Q alisema kwamba,kumekuwa na ongezeko la watu kutoka nje wanaokuja kufanya utafiti kwenye muziki huu na kuondoka nao lakini waandishi na wadau wa sanaa wa ndani wamelala katika hilo na hawajaona fursa hiyo.

“Muziki huu una historia kubwa hapa nchini,watu wengi wanakuja kufanya utafiti,kuandika vitabu na kujizolea fedha.Hapa kwetu waandishi hawajaona haja ya kufanya hivyo.Wanaandika mambo madogo binafsi na kutojikita kwneye undani wa muziki huu”alilalamika Fid Q.

Aliongeza kwamba,kama juhudi za makusudi hazitaelekezwa katika kufanya tafiti na kutunza kumbukumbu za kutosha katika eneo hili,basi vizazi vitakosa kitu adhimu cha kukumbuka na kurithi.

“Tuna makundi mengi yalikuwepo kama Kwanza Unit na baadaye Hard Brastarz.Yalifanya kazi kubwa kusimamisha muziki huu hasa Hiphop nani anakumbuka? Tunahitaji kuweka mambo haya katika maandishi.Ni ajabu kukosa maandiko na tafiti katika mambo haya” alisisitiza

Kwa upande wake muasisi wa muziki huu na mwanzilishi wa moja ya makundi ya mwanzo katika muziki wa kizazi kipya la Kwanza Unit, Zavala alisema kwamba,wageni ndiyo wamekuwa wakihangaika na tafiti katika muziki huu lakini kwa waandishi wa nyumbani bado.

“Watu wanachota mamilioni katika kuandika miradi na tafiti kwenye muziki huu.Inashangaza hakuna waandishi waliokwisha kujitokeza kuandika vitabu na kufanya tafiti katika eneo hili linalovuta maelfu ya vijana” alilalamika Zavala.

Akihitimisha mjadala Katibu Mtendaji wa BASATA,Ghonche Materego alisema kwamba,ni vema waandishi na wasanii wakajikita katika eneo la muziki wa kizazi kipya kwani hakuna machapisho na vitabu vya kutosha.

Shambulio la 11 Septemba 2001


Shambulio la 11 Septemba, 2001 ni tarehe na mwaka uliotokea mashambulio manne ya pamoja yaliyofanywa na kikosi cha Kigaidi cha al-Qaida dhidi ya Marekani. Kwa mujibu wa taarifa za maofisa, yasemekana kwamba kikosi cha Al-Qaida waliziteka nyala ndege nne wakazitumia kama silaha wakigongesha ndege katika majengo mjini New York na Washington DC kwa makusudi. Karibuni watu 3,000 walipoteza maisha katika shambulio hilo.

 Ndege zilitumika kufanyia Ughaini huo

Mabaki ya Jengo la WTC.
1. American Airlines Flight 11, iliyotumiwa kugonga mnara wa Kaskazini mwa Jengo la Biashara la Kimataifa (World Trade Center) la mjini New York mnamo saa 8:46:30 asubuhi.
2. United Airlines Flight 175, ilitumiwa kugonga mnara wa Jengo la Biashara la Kimataifa (World Trade Center) la Kusini mnamo saa 9:02:59 asubuhi. Watu wengi waliona tukio la pili kwasababu habari zilikuwa tayari zishasambaa katika mji na kila kamera za televisheni zilikuwa zikielekezea macho yao huko katika eneo la tukio, na wakati huo huo ndege ya pili ikagonga tena mnara wa Kusini mwa Jengo hilo.
3. American Airlines Flight 77, ilitumiwa kugonga jengo la Pentagon la mjini Arlington, Virginia (karibu kidogo na Washington DC), mnamo saa 9:37:46 asubuhi.
4. United Airlines Flight 93, hii haikubahatika kugonga mahala popote pale, badala yake wakaiangusha chini mnamo saa 10:03:11 asubuhi. Yaaminika ya kwamba magaidi hao walikuwa wakitaka kuigonga ndege hiyo katika jengo la mji mkuu wa Marekani. Abiria walijaribu kuinyang'anya Ndege hiyo kutoka mikononi mwa magaidi hao lakini hawakufanikiwa. Na matokeo Ndege ikashia kuanguka karibu na mji wa Shanksville, Pennsylvania.

 Matokeo ya maafa hayo

Jumla ya watu waliokufa katika shambulio hilo ni 246. Magaidi 19 waliuawa wakati wa shambulio hilo. Minara yote miwili ya jengo la World Trade Center yalipamba moto baada ya shambulio. Mnara wa Kusini (yaani WTC 2) liliungua kwa muda wa dakika 56 kbla ya kuanguka na kuangamia kabisa.
Jengo la Kaskazini (WTC 1) liliungua kwa muda wa dakikar 102 nalo pia lilianguka. Kama jengo la WTC lilivyoanguka, sehemu na mmong'onyoko wa jengo hilo lilipelekea majengo mengine yaliyoyazunguka majengo hayo kushika moto na kuharibika pia. Kutokaa na uharibifu uliotokea, jengo la tatu la 7 World Trade Center (7 WTC), nalo likaanguka mnamo saa 5:20 jioni. Baadahi ya mamjengo mengine yaliharibiwa vibaya na hata kuangamia kabisa yaani.
Takriban watu watu 2,602 walipoteza maisha katika Jengo la World Trade Center.
Ndege iliyogonga Pentagon iligonga chini mwa upande wa Magharibi mwa jengo hilo. Kisha ikagonga mpaka katika nguzo tano zinazoshikiria jengo hilo la Pentagon. Shambulio hilo Pentagon liliuwa watu 125.
Watu 2,973 walikufa katika shambulio hilo, wakiwemo watu watu wa zima moto waliokuwa wakijaribu kuokoa maisha ya baadhi ya watu waliopatwa na balaa hilo.
Hili lilikuwa ndio shambulio kubwa la kwanza kwa watu ambao wasio Waamerika kushambulia nchini humo tangu mnamo mwaka wa 1941, pale Wajapani waliposhambulia kituo cha jeshi la maji kilichopo katika Bandari ya Pearl, Hawaii. Dhana nyingi zilikuwa zikionekana kwamba kuna watu katika Marekani walikuwa wakijua kwamba kutatokea na tukio kama hilo kabla na ni lini itakuwa hivyo.

 Vita dhidi ya ugaidi

Baada ya shambulio, Wamarekani wakawa wanawalaumu Al-Qaeda kwa kitendo walicho kifanya. Tangu hapo wakaianza vita dhidi ya Ugaidi. Kiongozi wa al-Qaeda, Osama bin Laden, Alikimbilia nchini Afghanistan. Serikali ya Marekani iliwaambia Serikali ya Afghanistan, iitwayo Taliban, kumsalimisha bin Laden mikononi mwao. Wataliban hawakufanya hivyo. Kiongozi wa Wataliban, Mullah Muhammad Omar, aliitaka Serikali ya Marekani impe Uthibitisho unaonyesha kwamba Osama anahusika na tukio hilo. Rais wa Marekani bwana George W. Bush akasema kwamba hakuna haja kutaka Uthibitsho wowote ule na Serikali ya Marekani ikaanzisha vita dhidi ya Afghanistan.

Wednesday, June 29, 2011

Historia ya GaddafiKanali Muammar Gaddafi ni kiongozi aliyekaa madarakani kwa muda mrefu zaidi barani Afrika na katika nchi za Kiarabu.

Gaddafi
Gaddafi

Ameongoza Libya tangu alipompindua Mfalme Idris I, katika mapinduzi yasiyo ya kumwaga damu, wakati huo akiwa na umri wa miaka 27.
Maarufu kwa nguo anazopenda kuvaa, na walinzi wa kike wenye kubeba silaha, kiongozi huyo wa Libya pia anadhaniwa kuwa na mbinu nzuri za kisiasa, kwa kuweza kuirejesha Libya kutokana na kutengwa kidiplomasia duniani.
Baada ya miongo miwili ya kutengwa katika jamii ya kimataifa, mwaka 2003, Tripoli ilikiri kuwa walifanya shambulio la Lockerbie kwa kuiangamiza kwa mabomu ndege ya Pam Am na hapo Umoja wa Mataifa ukaondoa vikwazo dhidi ya Libya.
Gaddafi mwaka 1969
Gaddafi mwaka 1969

Baada ya miezi kadhaa, serikali ya Kanali Gaddafi ilisitisha mipango yake ya kuunda silaha za maangamizi na hii ikarejesha ushirikiano na nchi za magharibi.
Hapo ndipo mabadiliko halisi yalionekana kwa kuwa nchi hizo za magharibi zilibadili mtazamo wao na kuacha kumtenga Gaddafi na kushirikiana naye hata kama alikuwa hatabiriki.
Ni mtu wa kipekee katika kauli zake, mienendo yake, tabia zake na mikakati yake, kwa mujibu wa Saas Djebbar mtaalam wa siasa za Libya.
'Lakini ni mwanasiasa mashuhuri; hakuna shaka lolote kuhusu hilo. Ni mwanasiasa anayeweza kuhimili misukosuko ya kisiasa kwa hali ya juu sana.'

Asili ya Mabedui

Muammar Gaddafi alizaliwa jangwani karibu na Sirte mwaka 1942.
Gaddafi katika mkutano Sirte
Gaddafi katika mkutano Sirte

Alipokuwa kijana alivutiwa na kiongozi mzalendo wa Misri na, Gamal Abdel Nasser, alipokuwa akishiriki katika maandamano dhidi ya Israel wakati wa mtafaruku wa Suez mwaka 1956.
Gaddafi alipanga njama ya kupindua utawala wa kifalme alipokuwa mwanafunzi wa kijeshi na aliwahi kupata mafunzo zaidi akiwa Uingereza kabla ya kurejea nyumbani Libya, mji wa Benghazi, na kupanga mapinduzi ya tarehe 1 Septemba mwaka wa 1969.
Ghaddafi alianza kujenga itikadi zake za kisiasa mwaka 1970 na kuziandika katika kitabu chake cha kijani kibichi.
Gaddafi alipokuwa akizuru Senegal mwaka 1985
Gaddafi alipokuwa akizuru Senegal mwaka 1985

Alikitumia kitabu chake kuanzisha mfumo wa kisiasa iliyojumuisha kanuni za kiislamu na mfumo uliyo tofauti na siasa za ujamaa au ubepari.
Mwaka1977 aliasisi mfumo ujulikanao kama 'Jamahiriya' au 'Taifa la Umma' ambapo raia ndio wanaoendesha uongozi wa nchi yao kupitia 'kamati za umma'.
Hema ya Gaddafi
Hema ya Gaddafi

Mfumo huo wa Gaddafi umevuka mipaka na hauhusishi mambo ya siasa tu, bali pia mambo mengine.
Akiwa safarini ng'ambo, huwa anakaa kwenye kambi iliyojengwa na hema yake ya kifahari ya Kibeduwi akiwa amefuatana na walinzi wanawake ambao, inasemekana, huwa hawapotezi umakini kazini kama walinzi wanaume.
Hema hiyo pia hutumiwa kuwalaki wageni wa Libya na Kanali Gaddafi huendesha mikutano na mahojiano yake humo humo akipepea usinga au tawi la mitende.

Upekepeke

Benjamin Barber, mtaalam wa kisiasa wa kujitegemea, kutoka Marekani amewahi kukutana na Gaddafi mara kadhaa hivi karibuni na kuzungumza naye kuhusu mustakabali wa Libya.
Gaddafi akiwa na viongozi wengine wa nchi za Uarabuni
Gaddafi akiwa na viongozi wengine wa nchi za Uarabuni

Bw Barber alisema kuwa Muammar Gaddafi anajihisi kuwa msomi aliyebobea.
Muammar Gaddafi na Tony Blair waliwahi kuandaa mkutano wa viongozi kutoka nchi mbalimbali tarehe 29 Mei 2007 kwenye hema hiyo ya Kibedui.
"Utashangazwa kuwa ingawaje ni dikteta, ni mwanafalasafa na mwenye kutafakari jambo kabla ya kuzungumza," aliiambia BBC.
"Namchukulia sana kama mtu kutoka kabila la Waberber na mtu ambaye aliibuka kutoka tamaduni za watu wa jangwani, kutoka kwenye mchanga na kwa namna fulani kuna tofauti kubwa na uongozi wa kisasa, na kwa namna fulani hilo limemfanay awe mstahamilivu na mwenye msimamo."
Kanali Gaddafi amejitahidi kwa muda mrefu kutoa ushawishi wake nyumbani na ng'ambo.
Awali alituma jeshi lake nchini Chad ambapo wanajeshi walidhibiti ukanda wa Aozou, kaskazini mwa nchi hiyo, mwaka 1973.
Katika miaka ya 80 aliandaa mafunzo kwa makundi ya waasi kutoka Afrika Magharibi yaliyojumuisha wale wa Tuareg ambao ni Waberber.
Hivi karibuni aliongoza jitihada za kuwapatanisha waasi wa Tuareg kutoka nchi za Niger na Mali.

'Mbwa kichaa'

Jumuiya ya wanadiplomasia kuitenga Libya kulitokana na Kanali Muammar Gaddafi kuunga mkono makundi yeneye silaha, ikiwemo Irish Republican Army na Palestine Liberation Organisation.
Gaddafi akiwa na mwandishi wa habari wa BBC
Gaddafi akiwa na mwandishi wa habari wa BBC

Rais wa zamani wa Marekani Ronald Reagan alimwita Gaddafi 'mad dog' yaani 'mbwa kichaa' na Marekani ililipiza kisasi dhidi ya Libya kwa madai ya kuhusika na mashambulio ya anga barani Ulaya kwa kuvamia miji ya Tripoli na Benghazi mwaka 1986.
Ilisemekana kuwa Kanali Gaddafi alitikiswa na mashambulio ya mabomu hayo ambapo mtoto wake wa kike wa kufikia aliuawa.
Aliposhindwa katika jitihada zake za kuzipatanisha nchi za Uarabuni katika miaka ya 90, Kanali Gaddafi alielekeza nguvu zake barani Afrika na kupendekeza 'Muungano wa Nchi' za bara la Afrika.
Muuguzi wa Gaddafi
Muuguzi wa Gaddafi

Alianza kuvaa mavazi yake binafsi, sare za michezo zilizo na ngao za bara la Afrika au picha za viongozi kutoka bara hilo.
Wakati wa mabadiliko katika karne ya 20, huku Libya ikiwa inapata tabu kutokana na vikwazo dhidi ya nchi hiyo, alianza kurekebisha hali nchini mwake.
Mwaka wa 2003, mabadiliko yakaanza kuonekana na baada ya miaka mitano mkataba wa kulipa fidia kwa waathirika wa Lockerbire uliafikiwa na hii ikarejesha uhusiano kati ya Washington na Libya.
'Hakutakuwa na vita tena, mashambulio, na vitendo vya ugaidi' Kanali Gaddafi alisema alipokuwa akiiherehekea miaka 39 aliyokaa madarakani.

Changamoto za ndani


Kiongozi huyo wa Libya hujiona kama kiongozi wa kidini wa taifa hilo, akihakikisha kwa kile anachosema ni demokrasia.
Waandamanaji wa hivi karibuni Libya
Waandamanaji wa hivi karibuni Libya

Lakini katika hali halisi, wakosoaji wanasema Kanali Gaddafi amefanikiwa kudhibiti nchi hiyo.
Wanaompinga wamekandamizwa kikatili na vyombo vya habari vinabaki katika udhibiti mkubwa wa serikali.
Libya ina sheria ambazo haziwaruhusi watu kukusanyika katika misingi ya kisiasa zinazopinga mapinduzi ya Kanali Gaddafi.
Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch limesema serikali hiyo imewatia mbaroni mamia ya raia kwa kukiuka sheria hiyo na baadhi yao kuhukumiwa kifo.
Imeripotiwa kumekuwa na matukio ya utesaji na hata watu kupotea
Inadhaniwa kuwa Kanali Gaddafi anaandaa namna ya kukabidhi madaraka yake kwasababu ya umri aliyofikia sasa lakini haijulikani ni nani atakayerithi uongozi wa Libya kutoka kwa Gaddafi.
Sayf akiwa na ndugu yake Saad
Sayf akiwa na ndugu yake Saad

Kuna hisia kuwa mwanawe Sayf Al-Islam Gaddafi ndiye atarithi uongozi kutoka kwa baba yake na anaongoza katika kuleta mabadiliko.
Ingawaje Sayf ametangaza kuwa anastaafu siasa lakini kuna wanaohisi kuwa hii ni mbinu ya kuongeza ushawishi wake kisiasa.
Wakati huo huo, Gaddafi ameahidi kuwa wizara za nchi hiyo zitafutwa pamoja na bajeti zao
Utajiri utakaopatikana kutokana na mafuta utakabidhiwa moja kwa moja kwa wananchi.
Licha ya uchumi wa Libya kutoa fursa kwa wawekezaji wa nje, mabadiliko bado yanakwenda taratibu.
Waandamanaji wakichana picha ya Gaddafi
Waandamanaji wakichana picha ya Gaddafi

Walibya wengi wana wasiwasi juu ya mabadiliko yanayotokea na kuhisi kuwa hawapati manufaa kutoka rasilmali ya Libya, waangalizi wanasema kwani huduma za serikali ni duni pamoja na ubadhirifu mkubwa wa mali.
' Wanajihadhari sana katika mapambano hayo kwa kuwa hawataki mabadiliko yatakayolegeza nguvu za umma,' alisema Saad Djebbar
'Lakini wakati huo huo, Walibya wanafahamu kuwa wanahitaji kufanya mabadilko. Na ndio maana wanaenda taratibu sana.
Mfuasi wa Gaddafi
Mfuasi wa Gaddafi