"Hapa Arusha KILA HOSPITALI IMEPOKEA WATU WA MAGONJWA YA PRESHA, KISUKARI, PUMU, N.K. AMBAO WALIKWENDA LOLIONDO "KUTIBIWA" MARADHI HAYO NA BAADA YA KUPATA "NAFUU" (PSYCHOLOGICAL) KWA KAMA WIKI MBILI TU WAMEANZA KUUMWA SERIOUSLY NA KURUDIA DAWA ZAO ZA HOSPITALI TENA.

Pili, mimi nikiwa mfanyakazi wa maabara ya hospitali ya MT Meru, sijaona hata mgonjwa mmoja wa ukimwi aliyepata "seroconversion" yaani kurudi "seronegative from serpositive status". Kinachosikitisha ni kuwa kuna watu hawataki kabisa kusikia yanayosemwa na madaktari na wafanyakazi wa hospitali mbalimbali hapa Arusha ambao kila siku tuna-deal na watu wanaozidiwa baada ya kwenda Loliondo.


Mbaya zaidi kuna magazeti, tv na redio hayataki kabisa kusikia ukweli wa majanga yaliyowafika watu waliokwenda huko. Ajabu pia ni kuwa kuna watu ambao ukitaka kuwaeleza ukweli wanakuona wewe ni mpagani usiyemwamini Mungu. Naomba waandishi wa habari wawe proactive katika kutafuta ukweli na si kutegemea mass hysteria iliyowakumba maelfu ya watu wanaotafuta miujiza kwa nguvu."

Source: MJENGWA - Picha, Habari & Matangazo: Kama Haya Ni Ya Kweli