Tuesday, June 28, 2011

Andre Villas Boas kocha mpya wa Chelsea atangaza kuendeleza kasi yake katika klabu hiyo

Muda mfupi baada ya kuwasili Chelsea, Villas Boas alisema anataka kuendelea na kasi yake aliokuwa nayo na timu ya Porto na kushinda vikombe.
Kocha huyo mpya wa Chelsea, Andre Villas Boas alisema katika mkutano wake wa kwanza na vyombo vya habari kuwa lengo lake lilikuwa ni kushinda vikombe na hii ndiyo sababu anaelekea kujenga timu ya ushindini:
Kocha huyo alinukuliwa akisema"Hakuna shaka kwamba changamoto kubwa kwangu ni kuendelea kushinda. Mimi ni mtu mwenye kiu ya ushindi na mafaanikio natumai kuendelea hivyo. Tunataka kutengenza timu yenye nguvu. ni lazima kutafakari juu ya mafanikio ya klabu katika misimu sita iliyopita, kiwango cha kufikiwa na nini tunaweza kufanya kwa sasa na katika miaka ijayo
Mshindi wa msimu uliopita na wa kihistoria akiwa na klabu Porto (michuano, Kireno Super Cup, Kombe la Ligi na Europa), kocha huyo mwenye umri wa miaka 33, kasi yake imeongezeka mithili ya mwanga wa juwa. Mwaka (2009-2010): Académica Coimbra, 2010-2011: FC Porto, 2011-2012: Chelsea). Kama wasemavyo wataalamu sidhani kama kupanda kwa kasi kwa sifa ya kocha huyo hakuwezi kusitisha mfaanikio yake.
 Baada ya timu hiyo ya Chelsea kufanya kufuru ya usajili wa makocha, kocha huyo mpya sasa anafkiri kumsajili Mshambuliaji wa Inter milan Samuel Etoo Fils kwa kitita cha Yuro milioni 30 na mshabara wa milioni 10. samauel Etoo Fils ikiwa makubaliano yatafikia kikomo, ataungana kwenye mstari wa ushambuliaji na Fernando Torres. Tayari Samuel Etoo ameshaonyesha nia yake ya kumalizia msimu wake katika ligi ya Uingereza
Ujio wa Samuel Etoo Chelsea unaashiria kuondoka kwa Didier Drogba au Nicolas Anelka ambapo timu ya Inter milan imependekeza euro Milioni 10 kwa Nicolas Anelka

No comments:

Post a Comment