Friday, September 16, 2011

Kutumia kondom ya wanaume


kondom
Kondom ya wanaume
Mimi mvulana, mimi ni mwanamme nieleze jinsi ya kutumia kondom ya wanaume?
  • Hakikisha umeangalia mda wa matumizi wa kondom uliyonayo. Kama mda wake (expiry date) wa matumizi umekwisha basi haikufai. Fungua kipakiti chenye kondomu wakati tu ukiwa tayari kuitumia. Bila hivyo yale mafuta mafuta maalum kwenye kondomu yatakauka.
  • Unapofungua pakiti kuwa mwangalifu usiipasue, au kuitoboa wala kuiharibu kondom yenyewe. Ikipasuka itupilie mbali na uchukue nyingine.
  • Kondomu huwa zimesokotwa na kuwa kama duara. Kuivaa, ile sehemu ya mafuta mafuta inapaswa kuwa nje.
  • Hivyo basi ivae kwa kuikunjua kuanzia kwenye ncha (kichwa)cha uume.
  • Ishike sehemu ya chuchu ya kondomu kwa kutumia dole gumba na kidole chako cha kwanza ili kutoa hewa kutoka sehemu hiyo, ili manii yahifadhiwe mahali hapo pale yatakapotoka.
  • Sasa Endelea kuishikilia kondom kwa mkono mmoja. Kwa kutumia mkono wa pili ikunjue hadi kufikia kwenye mavuzi yaani kwenye shina la uume. Kama mtumiaji hajatahiriwa anapaswa kuvuta lile govi la uume wake kabla ya kuvaa kondomu. Kama kondomu haina kilainishi cha kutosha, vilainishi au majimaji (kama vile silicone, glycerine, au K-Y jelly) vyaweza kuongezwa kwa nje. Tahadhari mafuta kama yale ya kupikia, ya kujipaka mwilini kama kama vile Vaseline hayafai kutumiwa kama kilainishi.
  • Baada ya kufanya mapenzi kondomu inapaswa kuvuliwa kwa njia sahihi pia. Baada tu ya kufika kilele na kutoa manii, mwanaume anapaswa kuutoa uume wake kutoka ukeni, kabla haujalegea kabisa, kwani akichelewa huenda kondom ikatumbukia ukeni mwa mwanamke. Kisha ashikilie kondomu kutoka shinani mwa uume na kuivua taratibu pasi na manii kumwagika.
  • Unaweza kuifunga kondom kwenye karatasi na kuitupa kwenye choo cha shimo
  • Usitupe kondom kwenye hooni cha kupiga maji kwani huenda ikatatiza utendaji kazi wa choo hicho.
  • Tumia kondom nyengine kwa kila tendo jengine la kujamiana. Tumia kondom kila wakati unapofanya mapenzi.

Wednesday, August 24, 2011

Nasri aenda Man City

 Nasri
Manchester City wamekubaliana na Arsenal kumsajili kiungo Samir Nasri. Nasri sasa anaelekea mjini Manchester kwa ajili ya vipimo vya afya.
 
Nasri

Nasri alifanya mazoezi na Arsenal siku ya Jumanne asubuhi kujiandaa na mchezo wa Klabu Bingwa Ulaya dhidi ya Udinese, utakaochezwa Jumatano. Hata hivyo jina lake liliondolewa kwenye orodha ya wachezaji.
Kiungo huyo kutoka Ufaransa anakwenda Manchester pia kukamilisha mkataba wake ambao unadhaniwa kuwa na thamani ya pauni milioni 25.
Meneja wa City, Roberto Mancini alisema siku ya Jumapili kuwa anataka kumsajili Nasri ndani ya kipindi cha saa 48.
Nasri aenda Man City
Manchester City wamekubaliana na Arsenal kumsajili kiungo Samir Nasri. Nasri sasa anaelekea mjini Manchester kwa ajili ya vipimo vya afya
Nasri alifanya mazoezi na Arsenal siku ya Jumanne asubuhi kujiandaa na mchezo wa Klabu Bingwa Ulaya dhidi ya Udinese, utakaochezwa Jumatano. Hata hivyo jina lake liliondolewa kwenye orodha ya wachezaji.

Kiungo huyo kutoka Ufaransa anakwenda Manchester pia kukamilisha mkataba wake ambao unadhaniwa kuwa na thamani ya pauni milioni 25.

Meneja wa City, Roberto Mancini alisema siku ya Jumapili kuwa anataka kumsajili Nasri ndani ya kipindi cha saa 48.

Uholanzi yaipiku Hispania ubora wa soka

Uholanzi imeipiku Hispania katika nafasi ya kwanza ya ubora Fifa wa kusakata soka duniani, huku Englan ikipanda nafasi mbili juu hadi ya nne.
Wachezaji wa Uholanzi
Wachezaji wa Uholanzi

Hispania mabingwa wa soka duniani na Ulaya, wameporomoka hadi nafasi ya pili baada ya kupoteza pointi katika mchezo wa kirafiki dhidi ya Italia.
England, licha ya mchezo wake wa kirafiki dhidi ya Uholanzi kuahirishwa, imepanda kwa sababu Brazil ilifungwa na Ujerumani.
Jamhuri ya Ireland imepaa nafasi mbili hadi ya 31, Scotland imeruka nafasi sita na sasa inashikilia nafasi ya 55, Ireland Kaskazini nayo imefanikiwa kwenda nafasi tatu zaidi hadi ya 59, lakini Wales imeporomoka hadi nafasi ya 117.
Kwa kushika nafasi hiyo ya kwanza kwa mara ya kwanza, Uholanzi inakuwa ni taifa la saba kushikilia nafasi hiyo ya juu kisoka duniani zikiwemo - Argentina, Brazil, Ufaransa, Ujerumani na Italia ambazo ziliwahi kukalia kiti hicho.
Hispania ilikuwa inashikilia nafasi ya juu tangu mwezi wa Julai mwaka 2010 kufuatia ushindi walioupata wa Kombe la Dunia dhidi ya Uholanzi nchini Afrika Kusini.
Ujerumani inashikilia nafasi ya tatu, wakati Uruguay ndiyo nchi ya Amerika Kusini iliyo nafasi ya juu kwa dunia ikishika nafasi ya tano kutokana na kushinda Kombe la Copa America hivi karibuni nchini Argentina, wakati Brazil ipo nafasi ya sita.
Italia, Ureno, Argentina na Croatia wamefanikiwa kushikilia nafasi 10 za juu.
Viwango vya ubora wa soka vya Fifa vinatokana na kukusanya matokeo, umuhimu wa mechi zilizochezwa na ubora wa timu pinzani.

Thursday, July 14, 2011

Eritrean Red Sea FC footballers 'disappear' in Tanzania


Thirteen members of an Eritrean football team have failed to return home after a regional tournament in Tanzania, officials say.
After Red Sea FC lost the Cecafa championship semi-final on Saturday, only half of the team turned up for the return flight to Eritrea.
This is said to be the fourth time Eritrean footballers have disappeared.
Young Eritreans often try to escape poverty, a repressive government and national military service.
Tanzania Football Federation (TFF) Angetile Osiah told Reuters news agency that the matter had been reported to the law enforcement authorities to investigate.
"Some team members colluded in the incident by trying to stamp the passports of the missing players at airport immigration checkpoints but when a physical head count was conducted, it was discovered that 13 players were missing," he said.
Tanzania's Young Africans beat their rivals Simba 1-0 in Sunday's Cecafa final.

ROSTAM AZIZ Ajivua Ubunge Na Ujumbe wa NEC ya CCM.

 


ROSTAM ametangaza uamuzi huo katika mkutano uliofanyika IGUNGA  Jumatano wiki hii  ambapo amesema hatua hiyo haitokani na kile alichokiita kuwa ni shinikizo ndani ya chama, bali ni dhamira yake binafsi ikiwa na lengo la kutoa fursa kwa watu wengine kushika nyadhifa hizo alizoziacha.
Alitangaza uamuzi huo katika mkutano  uliofanyika huko IGUNGA TABORA ambapo pamoja na mambo mengine alieleza historia yake katika uongozi ndani ya CCM ukiwemo ubunge wa jimbo la IGUNGA alioushika tangu mwaka 1995 huku akitaja mafanikio na changamoto alizokumbana nazo.
Baadhi ya watu waliokuwa wamehudhuria mkutano huo  walijaribu kumsihi  AZIZ abadili uamuzi wake, suala ambalo alilipinga na kuendelea kushikiria msimamo wake.
Hata hivyo ofisi za Bunge kupitia kwa Kaimu Katibu wake JOHN JOEL zimesema hazina taarifa.
Safari ya siasa ya ROSTAM AZIZ ndani ya bunge ilianzia mwaka 1995 katika uchaguzi mkuu wa kwanza chini ya mfumo wa vyama vingi vya siasa ambapo aliibuka mshindi katika jimbo la IGUNGA.
Mwaka 2000 vile vile alitetea kiti chake cha ubunge na mwaka jana alishiriki katika kinyang’anyiro na katika mkutano wa kampeni wa mgombea wa kiti cha Urais kupitia CCM, Dkt. JAKAYA KIKWETE, aliweza kunadiwa.
Ndani ya Chama Cha Mapinduzi, ROSTAM aliwahi kuwa mjumbe wa Kamati Kuu ya halmashauri kuu ya taifa ya chama hicho, mjumbe wa NEC na mweka hazina.
Mwishoni mwa kikao cha halmashauri kuu ya taifa ya CCM kilichofanyika mjini DODOMA mwezi Aprili mwaka huu, Kamati Kuu ilijiuzulu na hivyo kutoa nafasi ya kuundwa kwa Kamati Kuu nyingine ambamo ROSTAM na wajumbe wengine kadhaa waliachwa
Mwanasiasa huyu pia ni mfanyabiashara ambapo kwa mujibu wa taarifa zilizochapishwa katika tovuti ya Bunge, Rostam ni Mkurugenzi katika kampuni za African Tanneries, Caspian construction, African Trade Development na katika kampuni ya Research on Business yeye ni Mkurugenzi Mtendaji.
Halikadhalika tovuti hiyo inaonyesha kuwa kielimu, ROSTAM ana shahada ya kwanza ya Uchumi
Mbunge wa IGUNGA kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi ROSTAM AZIZ
Mbunge wa IGUNGA kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi ROSTAM  AZIZ ametangaza kuachia nafasi za uongozi wa kisiasa alizokuwa akishikilia ukiwemo ubunge wa jimbo la IGUNGA mkoani TABORA ambao ameushikilia kwa takribani miaka 15  pamoja na ujumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho.

Wednesday, July 13, 2011

EPIQ NATION YAFANA COCOBEACH


Jumapili, iliyopita kampuni ya Simu za Mkononi ya Zantel kupitia Bidhaa yake mpya ya EPIQ NATION iliandaa tamasha kabambe la muziki pale Coco beach kwa ajili ya vijana. 
Wasanii mbalimbali walikuwepo kutoa burudani ikiwemo Mwasiti, Diamond, Chidi Benz na Nameless Kutoka Kenya. Pia kulikuwa na ma underground kibao waliopewa fursa ya kuonyesha vipaji vyao vya kuimba, kuchana pamoja na kudansi Diamond akiwa jukwaani

Saturday, July 9, 2011

Afrika yapata taifa jipya la Sudan Kusini

sherehe Sudan Kusini
Jumamosi hii Julai 9 mwaka 2011 ni siku itakayoingia katika vitabu vya historia kote duniani baada ya machafuko ya takriban miongo miwili hatimaye moja ya nchi kubwa kabisa barani Afrika Sudan inagawanywa rasmi mapande mawili Kaskazini inayosalia kuwa Sudan na taifa jipya linalozaliwa Sudan Kusini. Umoja wa Mataifa , Jumuiya ya kimataifa , Wahisani, Mashirika ya Umoja wa Mataifa na dunia nzima imeelekeza macho na masikio Juba mji mkuu wa taifa la 54 barani Afrika na Sudan yote kwa jumla , kuona historia ikiandikwa lakini kubwa zaidi nini kitakachofuata baada ya kujitawala.
Umoja wa Mataifa umejiandaa vilivyo kuhakikisha usalama umedumishwa ukizingatiwa kuna changamoto nyingi katika taifa hilo lililosambaratika na machafuko ambapo hadi sasa suala la Kordofan Kusini na Abyei yaliyoko mpakani yanatia mashaka. Kuchambua kwa kina histotia hii, matarajio na changamoto , mkuu wa idhaa hii Flora Nducha amezungumza na Dr Salim Ahmed Salim anayeifahamu vilivyo historia ya Sudan, aliyewai kuwa Katibu mkuu wa Umoja wa Afrika na mpatanishi maalum wa Umoja wa Afrika katika mzozo wa Darfur.

Friday, July 8, 2011

Haye atakiwa marekani

Haye atakiwa Marekani
Friday, 08 July 2011 06:41
LOS ANGELES, Marekani

DAVID Haye, ameambiwa aende kupigana Marekani ili apate mafanikio kama bondia mwingine wa Uingereza, Amir Khan.Khan alikwenda kufanya mazoezi Marekani na akaja kuwa bingwa wa dunia baada ya kwenda Hollywood na kufanyishwa mazoezi na kocha mahiri wa Kimarekani, Freddie Roach.

Mtu maarufu katika ngumi, Richard Schaefer, anaamini kuwa kipaji cha Haye kinaweza kuzaliwa upya baada ya kupoteza pambano lake la uzito wa juu duniani kwa kupigwa kwa pointi dhidi ya Wladimir Klitschko, mjini Hamburg, Jumamosi usiku.

Haye sasa anataka kurudiana na Klitschko au kutwangana na kaka yake Vitali, ambaye ni bingwa wa mkanda wa WBC .

Lakini Schaeffer, ambaye ni Mtendaji Mkuu wa kampuni ya promosheni ya Oscar De La Hoya, Golden Boy, ambaye ni promota wa Khan na Haye alisema, "anatakiwa kuja na kupigana mapambano Marekani kwa mara ya kwanza.

"David hakuweza kucheza vizuri Jumamosi na sikufurahishwa na uchezaji wake.

"Lakini si sahihi kumjaji David kwa uchezaji wa mechi moja. Ana umri wa miaka 30 na bado ni mzuri, ni mpiganaji anayefurahisha katika uzito.

"Hakuna anayejali kuhusu akina Klitschkos."

Wakati huohuo, Schaefer, amesema Khan anaweza kujiandaa kupigana kwa ajili ya kutwangana na Floyd  Mayweather mwakani.

Bingwa wa mkanda wa WBA, Khan, ameanza maandalizi ya kucheza pambano la kuunganisha mataji dhidi ya Zab Judah mjini Las Vegas, Julai 23.

Pambano lake linalofuatia linaweza kuwa dhidi ya Erik Morales, Desemba na kisha kurejea Uingereza ambapo bondia huyo mwenye miaka 24, atahamia katika uzani wa welter na anaweza kutwangana na Kell Brook.

Huenda akatwanga na  Mayweather Novemba 2012.

Schaefer alisema: "Hii ni mipango mikubwa kwa Khan.

"Nimekuwa na mazungumzo na Mayweather na yuko tayari kutwangana na Amir."
 
Haye atakiwa Marekani
Friday, 08 July 2011 06:41
LOS ANGELES, Marekani

DAVID Haye, ameambiwa aende kupigana Marekani ili apate mafanikio kama bondia mwingine wa Uingereza, Amir Khan.Khan alikwenda kufanya mazoezi Marekani na akaja kuwa bingwa wa dunia baada ya kwenda Hollywood na kufanyishwa mazoezi na kocha mahiri wa Kimarekani, Freddie Roach.

Mtu maarufu katika ngumi, Richard Schaefer, anaamini kuwa kipaji cha Haye kinaweza kuzaliwa upya baada ya kupoteza pambano lake la uzito wa juu duniani kwa kupigwa kwa pointi dhidi ya Wladimir Klitschko, mjini Hamburg, Jumamosi usiku.

Haye sasa anataka kurudiana na Klitschko au kutwangana na kaka yake Vitali, ambaye ni bingwa wa mkanda wa WBC .

Lakini Schaeffer, ambaye ni Mtendaji Mkuu wa kampuni ya promosheni ya Oscar De La Hoya, Golden Boy, ambaye ni promota wa Khan na Haye alisema, "anatakiwa kuja na kupigana mapambano Marekani kwa mara ya kwanza.

"David hakuweza kucheza vizuri Jumamosi na sikufurahishwa na uchezaji wake.

"Lakini si sahihi kumjaji David kwa uchezaji wa mechi moja. Ana umri wa miaka 30 na bado ni mzuri, ni mpiganaji anayefurahisha katika uzito.

"Hakuna anayejali kuhusu akina Klitschkos."

Wakati huohuo, Schaefer, amesema Khan anaweza kujiandaa kupigana kwa ajili ya kutwangana na Floyd  Mayweather mwakani.

Bingwa wa mkanda wa WBA, Khan, ameanza maandalizi ya kucheza pambano la kuunganisha mataji dhidi ya Zab Judah mjini Las Vegas, Julai 23.

Pambano lake linalofuatia linaweza kuwa dhidi ya Erik Morales, Desemba na kisha kurejea Uingereza ambapo bondia huyo mwenye miaka 24, atahamia katika uzani wa welter na anaweza kutwangana na Kell Brook.

Huenda akatwanga na  Mayweather Novemba 2012.

Schaefer alisema: "Hii ni mipango mikubwa kwa Khan.

"Nimekuwa na mazungumzo na Mayweather na yuko tayari kutwangana na Amir."
 
DAVID Haye, ameambiwa aende kupigana Marekani ili apate mafanikio kama bondia mwingine wa Uingereza, Amir Khan.Khan alikwenda kufanya mazoezi Marekani na akaja kuwa bingwa wa dunia baada ya kwenda Hollywood na kufanyishwa mazoezi na kocha mahiri wa Kimarekani, Freddie Roach.

Mtu maarufu katika ngumi, Richard Schaefer, anaamini kuwa kipaji cha Haye kinaweza kuzaliwa upya baada ya kupoteza pambano lake la uzito wa juu duniani kwa kupigwa kwa pointi dhidi ya Wladimir Klitschko, mjini Hamburg, Jumamosi usiku.

Haye sasa anataka kurudiana na Klitschko au kutwangana na kaka yake Vitali, ambaye ni bingwa wa mkanda wa WBC .

Lakini Schaeffer, ambaye ni Mtendaji Mkuu wa kampuni ya promosheni ya Oscar De La Hoya, Golden Boy, ambaye ni promota wa Khan na Haye alisema, "anatakiwa kuja na kupigana mapambano Marekani kwa mara ya kwanza.

"David hakuweza kucheza vizuri Jumamosi na sikufurahishwa na uchezaji wake.

"Lakini si sahihi kumjaji David kwa uchezaji wa mechi moja. Ana umri wa miaka 30 na bado ni mzuri, ni mpiganaji anayefurahisha katika uzito.

"Hakuna anayejali kuhusu akina Klitschkos."

Wakati huohuo, Schaefer, amesema Khan anaweza kujiandaa kupigana kwa ajili ya kutwangana na Floyd  Mayweather mwakani.

Bingwa wa mkanda wa WBA, Khan, ameanza maandalizi ya kucheza pambano la kuunganisha mataji dhidi ya Zab Judah mjini Las Vegas, Julai 23.

Pambano lake linalofuatia linaweza kuwa dhidi ya Erik Morales, Desemba na kisha kurejea Uingereza ambapo bondia huyo mwenye miaka 24, atahamia katika uzani wa welter na anaweza kutwangana na Kell Brook.

Huenda akatwanga na  Mayweather Novemba 2012.

Schaefer alisema: "Hii ni mipango mikubwa kwa Khan.

"Nimekuwa nazungumza na myweather na yuko tayari kutwangana na Amir

Thursday, July 7, 2011

CCM Kuanza Kusherehekea Miaka 50 Ya Uhuru

 

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


Mwaka huu Sehemu ya nchi yetu, yaani Tanzania Bara itaadhimisha miaka hamsini ya Uhuru wake toka kwa Wakoloni. Uhuru huu uliopatikana miaka hamsini iliyopita ni kazi nzuri na ya Kizalendo iliyofanywa na Chama cha TANU.

Chama Cha Mapinduzi katika kukumbuka kazi hii nzuri ya kutafuta Uhuru wa nchi yetu kimeamua kufanya shughuli mbalimbali za kukumbuka kuzaliwa kwa chama kilicholeta Uhuru wa Tanzania Bara yaani TANU.

Itakumbukwa TANU ilizaliwa tarehe 7/7/1954 hapa Dar es salaam katika mtaa wa New street ambao kwa sasa unafahamika kama mtaa wa Lumumba mahali ambapo sasa ni  Ofisi Ndogo ya CCM Makao Makuu. Huo ukawa ndio mwanzo wa harakati za kudai Uhuru, Utu na Heshima ya Mwafrika katika nchi yetu.

Kwa kuienzi historia na kazi nzuri na ya Kizalendo iliyofanywa na TANU, Chama Cha Mapinduzi kimeamua katika kuadhimisha miaka hamsini ya Uhuru wa Tanzania Bara kuandaa shughuli mbalimbali za kijamii zikiwa na kauli mbiu Uhuru na Kazi, kauli maarufu katika miaka ya nyuma ambayo Baba wa Taifa Mwalimu J. K. Nyerere aliitoa katika hotuba yake ya kusisimua siku ya mkesha wa Uhuru wa Tanganyika mwaka 1961.

Mwalimu Nyerere aliitumia hotuba hiyo kuwaeleza wananchi wajiandae kuanza kufanya kazi kwa bidii ili kujiletea wao wenyewe na nchi maenedeleo. Maadhimisho haya yatafanyika nchi nzima kuanzia ngazi za matawi na kuwashirikisha wanachama wetu na wananchi wote kwa ujumla. Shughuli zitakazofanyika ni kama zifuatavyo:-

     i.        Usiku wa kuamkia tarehe 7/7/2011 Vijana wa CCM nchini watakutana maeneo mbalimbali kufanya shamrashamra za kuzaliwa TANU

    ii.        Tarehe 7/7/2011 asubuhi wanachama wa CCM na wananchi watakutana kwenye matawi yao na kufanya shughuli mbalimbali za kijamii kama vile, kufanya usafi, kusaidia ujenzi, kupanda miti, kutembelea wagonjwa mahospitalini n.k.

  iii.        Ikiwezekana kufanya matamasha mbali mbali yatakayowashirikisha vijana wasomi wanasiasa na wazee kujadili masuala mbali mbali yenye faida kwa Kata, Wilaya, Mkoa au Taifa kwa ujumla.

  iv.        Kufanya mikutano ya hadhara na kujikumbusha mafanikio yaliyopatikana kwa kila Mkoa na  Wilaya katika kipindi cha miaka 50 ya Uhuru.

Kwa Sehemu kubwa tunategemea walezi wa CCM wa Mikoa na Viongozi mbalimbali wa Kitaifa watashiriki shughuli hizo mikoani. Sherehe hizi zitaanza usiku wa tarehe 6/7/2011 kwa vijana wa CCM sehemu mbalimbali nchini kukutana na kusherehekea ikiwa ni pamoja na kufyatua MAFATAKI saa sita usiku ya siku hiyo, kama ishara ya kuzaliwa TANU.

Mwenyekiti wa CCM Taifa Dr. Jakaya M. Kikwete atashiriki sherehe hizi mkoani Dar es salaam, usiku wa Tarehe 06/07/2011 na tarehe 07/07/2011 asubuhi atakutana na Mabalozi wa Nyumba Kumi Mkoa wa Dar es salaam.

Ni mategemeo yangu vyombo vya habari vitashirikiana nasi katika kuuelimisha umma kuhusu historia hii muhimu ya Taifa letu na kutangaza matukio yote yatakayo ambatana na maadhimisho haya.

Wednesday, July 6, 2011

SIMBA YATINGA NUSU FAINALI KOMBE LA KAGAME

Wachezaji wa timu ya Simba wakishangilia baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Bunamwaya ya Uganda katika mchezo wa Robo Fainali Kombe la Kagame uliochezwa Julai 5,2011 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Kwa ushindi huo, sasa Simba imetangulia katika fainali hizo ambapo itamenyana na El Mereikh ya Sudan katika mechi ya nusu fainali mwishoni mwa wiki, ambapo El Mereikh ilikata tiketi hiyo baada kuifunga Ulinzi ya Kenya katika mchezo uliomalizika Julai 5,2011 kwa njia ya matuta

Saturday, July 2, 2011

Asema serikali imefanya maamuzi magumu



Mbunge wa Monduli (CCM), Edward Lowassa
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, amejibu hoja zilizotolewa na Mbunge wa Monduli (CCM), Edward Lowassa, wiki iliyopita kuwa serikali ya awamu ya nne imeshindwa kufanya maamuzi magumu, kwa kuorodhesha mambo mbalimbali ambayo yamesema ni magumu yakiwa yamechukuliwa na serikali.

 Pinda alisema hayo alipokuwa akijibu hoja za wabunge waliochangia mjadala wa bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka wa fedha wa 2011/2012, bungeni, mjini hapa jana jioni.  Lowassa akichangia mjadala wa bajeti hiyo wiki iliyopita, alisema kuna ugonjwa wa kuogopa kutoa maamuzi hivyo akataka serikali kutoa maamuzi na kusema: 

 “Heri ukosee kwenye kutoa maamuzi kuliko kutotoa maamuzi. Toeni maamuzi, acheni kuogopa, tumepewa nchi, tufanyeni maamuzi. Heri uhukumiwe kwa kutoa mamuzi kuliko kwa kutotoa maamuzi. Toeni maamuzi. Nasema tunaweza kufanya. Tukinuia, tukiamua, tunaweza kufanya.”

 Pinda alisema serikali ya awamu ya nne inayoongozwa na Rais Dk. Jakaya Kikwete ndiyo pekee imefanya maamuzi magumu na mazito kuliko serikali zote zilizopita.

 Alisema imekuwa ikifanya maamuzi thabiti na magumu, lakini kwa busara na tahadhari ili kutenda haki na kwa kuzingatia uwezo wake ili kulinda maslahi ya wananchi na kudumisha amani.

  Alisema katika kufanya maamuzi hayo, serikali imekuwa makini kuzingatia sheria, kanuni na taratibu.

 Aliyataja maamuzi magumu yaliyokwishafanywa na serikali ya awamu ya nne kuwa ni pamoja na kuwafikisha mahakamani waliokuwa mawaziri wa serikali zilizopita kutokana na tuhuma mbalimbali zinazowakabili za kutumia madaraka isivyo halali; na pia kujenga shule za sekondari za kata, ambazo zimewezesha wanafunzi wengi kupata elimu ya sekondari.

 Mengine ni kujenga Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom);  kujenga Chuo cha Serikali za Mitaa Hombolo; kukamilisha miradi yote 27 ya barabara kuu zilizoanzishwa na serikali ya awamu ya tatu; ujenzi na ukamilishaji wa miradi ya maji nchini; na kuwalinda watu wenye ulemavu wa ngozi (albino).

 Pia, kuondoa mpasuko wa kisiasa Zanzibar na kuanzisha serikali ya umoja wa kitaifa katika Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ); kupanua na kushamiri kwa demokrasia nchini kwa kiwango kikubwa; uhuru mkubwa wa vyombo vya habari; na kuruhusu kuanzisha mchakato wa kupata Katiba mpya. 

  “Lakini pia katika awamu hii ndipo tumefanya maamuzi mazito sana ya kuvunja Baraza la Mawaziri kufuatia kujiuzulu kwa aliyekuwa Waziri Mkuu, Mheshimiwa Edward Lowassa. Hili nalo halikuwa jambo jepesi hata kidogo. Inataka Moyo!” alisema Pinda.

Aliongeza: “... maisha ya serikali katika kutekeleza majukumu yake kwa dhana ya uwajibikaji wa pamoja kupitia Baraza la Mawaziri. Tunachohitaji ni kuvumiliana. Kuvuta subira, kwani mambo mema hayataki haraka!  Tutaamua na Tutafanya!”
 Akizungumzia suala la posho, alisema suala hilo ni muhimu kutazamwa kwa upana wake na kwa msingi ulioelezwa chini ya Mpango wa Miaka Mitano, yaani kuzungumzia posho zote.  

“Hii ni kwa sababu kwa mujibu wa Waraka wa Masharti ya Kazi za Mbunge; stahili za wabunge ni pamoja na zifuatazo: Mshahara wa mbunge kodi Sh. 588,000 ambao ulishakatwa, ambao haujakatwa kodi  ni Sh. 2,305,000, ukisakatwa kodi ni Sh. 1,717,000. Posho ya ubunge; posho ya vikao vya Bunge na kamati zake,” alisema Pinda.

  Aliongeza: “Posho ya madaraka kwa viongozi; Entertainment Allowance (posho za maburudisho) kwa viongozi; posho ya kujikimu ndani na nje ya nchi; posho ya mavazi anaposafiri nje ya Tanzania; posho ya msaidizi wa ofisi ya mbunge; posho ya usafiri wakati wa vikao vya kamati na mikutano ya Bunge; vilevile, kuna posho ya mafuta (Lita 1,000) kwa mwezi na Mfuko wa Maendeleo wa Jimbo (CDCF).”

 Pinda alisema kwa kuwa suala hilo lipo ndani ya Mpango wa Maendeleo, serikali italitafakari kwa undani na kuangalia posho zipi hazina tija na zipi zina tija na manufaa ya kuongeza ufanisi ili ikiwezekana zihuishwe na kujumuishwa ndani ya mishahara au vinginevyo kama itakavyoonekana inafaa.

 Alisema serikali pia itaangalia suala la kupunguza gharama za matumizi ya serikali kwa ujumla wake ikijumuisha kupunguza matumizi yasiyo ya lazima katika taasisi zote za serikali.

  Pinda alisema kwa maelekezo ya Rais Kikwete, uamuzi wa kuhamia Dodoma hauna budi kutekelezwa na kusisitiza kuwa hata kama fedha zimetengwa, Ofisi ya Waziri Mkuu itajengwa Dodoma.